Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Msitupe presha, wengi wetu tunaugua magonjwa mbalimbali, Seneta Ledama asema

Ec77e37bd832e377 Msitupe presha, wengi wetu tunaugua magonjwa mbalimbali, Seneta Ledama asema

Sat, 17 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Wakenya hutumia mtandao wa Twitter mara kwa mara kuwashambulia, kuwakosoa na kuwashtumu viongozi hasa wa kisiasa

- Hivi majuzi, Wakenya walizua mijadala mikali kuhusu madai kwamba serikali inapanga kuchukua mkopo wa KSh 276.7 bilioni kutoka kwa Shirika la Fedha duniani, IMF

- Akiwatetea viongozi wenzake, Senata wa Narok Ledama Ole Kina alisema wengine wao wanaugua magonjwa tofauti na hawapaswi kupewa presha

Seneta wa Narok Ledama Ole Kina amewarai Wakenya kuwawia radhi baadhi ya viongozi wa kisiasa ambao hawajakuwa wakitekeleza wajibu wao ipasavyo.

Kulingana na Ledama, baadhi ya viongozi wanaugua magonjwa mbali mbali na hawapaswi kushtuliwa wala kushinikizwa kufanya jambo lolote.

TUKO.co.ke inafahamu kwamba, mamia ya Wakenya hutumia mtandao wa Twitter kuwashambulia na kuwaanika wanasiasa ambao wanatepetea kazini.

'" Wanamitandao wa Twitter, tafadhalini kuweni wapole kwa waheshimiwa, wengi wetu sisi viongozi wa kisiasa huwa tunaugua magonjwa kadhaa ikiwemo ya kisukari, saratani, Ukimwi na hata ugonjwa wa shinikizo la damu, wengine wetu tukipata presha kidogo tunazimia," Ledama alisema.



Madai ya Ledama yanajiri wiki chache baada ya Wakenya kushambulia serikali kwa madai kwamba inapanga kuchukua mkopo wa KSh 276.7 bilioni kutoka kwa Shirika la Fedha la Dunia, IMF wa kukabiliana na janga la COVID-19.

" Hatutaki mikopo mingine zaidi, tayari sisi kama Wakenya tuna mizigo ambayo imetuzidi kubeba, serikali yetu ni fisadi kupindukia, tunajua pesa hizo zitawaendea wanasiasa badala ya wafadhiliwa, Tafadhali IMF sikia kilio cha mwananchi wa kawaida," Regina Matheka alisema.

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke