Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Msinibague kwa kuwa wakili wa Uhuru, Fred Ngatia aiomba JSC

854006aa3361eb90 Msinibague kwa kuwa wakili wa Uhuru, Fred Ngatia aiomba JSC

Tue, 20 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wakili Fred Ngati amesema uhusiano wake na Rais Uhuru Kenyatta haufai kumnyima nafasi ya kuwa Jaji Mkuu.

Alisema hayo wakati wa mahojiano ya jaji mkuu mtarajiwa Jumanne Aprili 20 alipofika mbele ya Tume ya Huduma za Mahakama (JSC).

"Msinibague kwa mujibu wa wateja ambao nimewahi kuwakilisha. Mnipige msasa kwa mambo mengine yote. Nimewahi kuwakilisha hospice, na kisha nikarudi kwenye kazi yangu ya kibinafsi baada ya kumwakilisha rais mteule 2013," alisema Ngatia.

Ngatia alisema walimalizana na Kneyatta baada ya kumuwakilisha na hajawahi kunufaika kwa vyovyote kwa sababu ya wajibu wake wa 203.



"Hakuna vile nimeweza kushawishiwa na rais. Sikupata uteuzi wa aina yoyote au kunufaika kwa sababu ya rufaa ya uchaguzi wa urais 2013. Nikipata nafasi hii nitafanya kazi yangu kwa uhuru katika idara ya mahakama," alisema wakili huyo.

Suala hilo lilikuwa ni mwiba kwa Ngatia huku kamishna akimwarifu Wakenya wana hofu kuwa yeye atakuwa kibaraka cha Rais Uhuru Kenyatta.

"Hakuna hata mrengo wa kisiasa ambao umeteta kunihusu. Kwa sababu wanajua Ngatia ni wakili mwenye bidii na asiyeegemea upande wowote. Mimi nina akili ya kibinafasi," aliendelea kujitetea.

Awali Ngatia alisisimua makamishna na falsafa alizosoma wakati wa kupata shahada ya uzamili.

Alisema yeye ni wakili mchapa kazi ambaye ataleta mageuzi makubwa ndani ya idara ya mahakama.

Aidha wakati wa mahojiano hayo Ngatia alisema yeye si mtu wa mitandao na hutumia wakati wake kwenye maktaba akisoma.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke