Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Msichana jasiri aendesha mashua usiku kumkimbiza mama mjamzito hospitalini

884ae877154f23b4 Msichana jasiri aendesha mashua usiku kumkimbiza mama mjamzito hospitalini

Thu, 20 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Virginia Aoko alisema mama yake Judith Anyango Akala, alimuamsha saa tisa asubuhi Jumanne, Mei 18, akiwa na uchungu wa kuzaa

- Alisema baba yake alikuwa amekwenda mbali kuvua samaki kwenye Ziwa Victoria

- Katika hatua ambayo imewashangaza wengi, msichana huyo usiku huo wa manane alimuomba mama yake apande mashua kisha alimuendesha hadi hospitalini

Msichana mwenye umri wa miaka 12, kutoka kijiji cha Rukala, kaunti ya Busia amekuwa maarufu baada ya kuendesha mashua usiku wa manane kwenye Ziwa Victoria kumkimbiza mama yake mjamzito hospitalini.

Virginia Aoko alisema mama yake Judith Anyango Akala, alimuamsha saa tisa asubuhi Jumanne, Mei 18, na uchungu aliyokuwa nao ulimfanya kuchukua hatua za haraka.

Akizungumza na Nation, Aoko alisema alifikiria kuwa kaka yake mdogo ambaye alikuwa anaugua malaria alikuwa anazimia ama kuna jambo lingine la dharura ambalo liliwahitaji kutoka kambini waliyohamia baada ya nyumba yao kusombwa na maji ya Ziwa Victoria.

Uchungu wa kuzaaHata hivyo, mwanafunzi huyo wa Darasa la Saba katika Shule ya Msingi ya Budala aligundua kwamba mama yake alikuwa na uchungu wa kuzaa na alihitaji matibabu ya dharura.

Huku baba yake akiwa amekwenda mbali kuvua samaki, msichana huyo alitambua kuwa maisha ya mama yake yamo mkononi mwake.

Katika hatua ambayo imewashangaza wengi, msichana huyo usiku huo wa manane alimuomba mama yake apande mashua kisha alimuendesha hadi hospitalini.

“Nilikuwa na wasiwasi kuwa endapo sitachukuwa hatua za haraka, atampoteza mtoto na huenda pia kufa kutokana na matatizo ya uchungu wa kuzaa," Virginia.

Licha ya magugu ya maji na baridi, msichana huyo jasiri alimuendesa mama yake kwa umbali wa kilomita mbili hadi Kituo cha Afya Rukala.

Alisema wauguzi wa hospitali hiyo walimsaidia mama yake kujifungua salama mtoto wa kiume.

“Sikutaka kumpoteza mama yangu na kuwa yatima. Pia nilijua endapo sitachukuwa tahadhari, huenda angelipoteza mtoto," aliongezea.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke