Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mshukiwa wa mauaji ya kimbari ya Rwanda akamatwa Uholanzi

Mshukiwa Wa Mauaji Ya Kimbari Ya Rwanda Akamatwa Uholanzi Mshukiwa wa mauaji ya kimbari ya Rwanda akamatwa Uholanzi

Tue, 3 Oct 2023 Chanzo: Bbc

Afisa wa zamani wa jeshi la Rwanda ambaye anashukiwa kuwa na jukumu muhimu katika mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994 amekamatwa Uholanzi siku ya Jumanne, waendesha mashtaka wa Uholanzi wamesema.

Pierre-Claver Karangwa, mwenye umri wa miaka 67, alikamatwa katika uchunguzi wa Uholanzi kuhusu jukumu lake katika mauaji ya kimbari, ambayo waendesha mashtaka waliuanza baada ya Mahakama Kuu ya Uholanzi mwezi Juni mwaka huu kusema kuwa hawezi kupelekwa Rwanda kwa hofu ya kwamba kesi yake isingekuwa ya haki.

Rwanda inamtuhumu Karangwa kwa kuhusika na mauaji ya Watutsi karibu 30,000 katika parokia ya Mugina karibu na mji mkuu wa Rwanda Kigali mwezi Aprili 1994 na iliomba apelekwe nchini humo mwaka 2012.

Katika kesi mahakamani kuhusu uwezekano wa kusafirishwa kwake Desemba 2022, Karangwa alisema hakuwa na hatia ya uhalifu aliotuhumiwa.

Karangwa, ambaye ameishi Uholanzi tangu 1998, alikuwa na uraia wa Uholanzi uliofutwa juu ya mashtaka ya mauaji ya kimbari.

Kinadharia hii inaruhusu kupelekwa kwake Rwanda, lakini Mahakama Kuu ilikanusha madai hayo kwa sababu Karangwa alikuwa mwanasiasa wa upinzani.

Waendesha mashtaka nchini Uholanzi wamesema wanamshuku Karangwa kwa kuhusika katika kuchoma nyumba na wanawake na watoto kadhaa waliokuwemo ndani yake kufuatia shambulio hilo katika parokia ya Mugina.

Takriban watu 800,000 wa kabila la Watutsi na Wahutu wenye msimammo wa kadri waliuawa wakati wa mauaji ya kimbari ya Rwanda, yaliyoongozwa na serikali ya Wahutu wenye itikadi kali.

Chanzo: Bbc