Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mshahara wa Shaffie Weru Wazua Hisia Mseto Kwenye Mtandao

99ab9165af0837f3 Mshahara wa Shaffie Weru Wazua Hisia Mseto Kwenye Mtandao

Thu, 1 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Wanamtandao walisema Shaffie alikuwa akilipwa kama mbunge na wala si mwanahabari

- Mshahara wake ulizua ucheshi mtandaoni haswa kutoka kwa Wakenya ambao hulipwa peanuts na simsims

- Shaffie alitishia kumshtaki aliyekuwa mwajiri wake kwa kumfuta kazi kiholela

Wakenya kwenye mtandao walibaki kinywa wazi baada ya mshahara aliokuwa akipata mtangazaji Shaffie Weru katika HomeBoyz Radio kufichuka.

Shaffie alikuwa akipokea zaidi ya nusu milioni kila mwisho wa mwezi kwa kuwa mtangazaji wa kipindi.

Kulingana na stakabadhi za malipo zilizoibuka mtandaoni, mtanagzaji huyo alikuwa akipata KSh 682, 500.

Hayo yalifichuka baada ya Shaffi kusema ataishtaki kampuni ya Radio Africa Group, ambayo inamiliki HomeBoyz Radio, kwa kumfuta kazi kiholela.

Shaffie alimtaka aliyekuwa mwajiri wake kumlipa takriban milioni 21 kwa kumfuta kazi la sivyo wakutane mahakamani.

Wakenya kwenye mtandao walibaki wakimeza mate baada ya macho yao kukwama hapo kwa mshahara wa Shaffie.

Otwero Bartholomew alisema hakuamini macho yake kwani alijua kitita kama hicho kinapokewa na wabunge peke yao..

Wengine nao walisema watakaochukua nafasi ya Shaffie watashtuka sana baada ya kuona alichokuwa akipokea na wao walikubali malipo ya chini.

Miss Rachel naye malipo ya Shaffie yalimkumbusha enzi zake na kusema ni tukio lililomchoma sana.

Wengi walitamani wangepata nafasi ya kupokea mshahara kama wa mtangazaji huyo ambaye anajulikana sana kwenye sekta ya usanii.

Shaffie huishi maisha ya juu na huenda mshahara huo kwake si ubwa kama walivyofikiria wanamtandao.

Hata hivyo, kwa wengi ambao hupokea mishahara midogo kiasi cha kuitwa Peanuts ama simsims, basi walibaki kumuenzi Shaffie.

Alipigwa kalamu na HomeBoyz baada ya mjadala wake hewani kudai kudhalilisha mwanamke huku ukiunga mkono hujuma dhidi ya kina mama.

Mamlaka ya mawasiliano nchini CAK tayari ilipiga redio hiyo faini ya KSh 1M kutokana na hulka za watangazaji wake na kuitaka kuomba msamaha kwa Wakenya wote.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke