Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Msanii Akon afanya mkutano wa kibiashara na Rais Museveni Ikuluni Entebbe

5a2ce1467ff89f53 Msanii Akon afanya mkutano wa kibiashara na Rais Museveni Ikuluni Entebbe

Wed, 19 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mwanamuziki Akon, mkewe na kikundi maalum cha wawekezaji walikutana na Rais Yoweri Museveni katika Ikulu ya Entebbe Jumatatu, Mei 17

- Habari za mkutano huo zilitangazwa na Rais Museveni kwenye mtandao wa Twitter

- Akon na Rais Museveni wanaripotiwa kujadili miradi tofauti ya uwekezaji ambayo mwanamuziki huyo anaamini itamuimarisha kibiashara Barani Afrika

Mwanamuziki nyota wa nyimbo aina ya RnB na mzaliwa wa Senegal ambaye pia ni raia wa Marekani Aliaune Damala Badara Thiam, maarufu Akon yuko nchini Uganda kwa ziara ya kibiashara.

Akon, mkewe Rozina Negusir pamoja na kikundi maalum cha wawekezaji walikutana na Rais Yoweri Museveni katika Ikulu ya Entebbe Jumatatu, Mei 17.

Maudhui ya mkutano huo yalikuwa ni kujadili miradi tofauti ya uwekezaji ambayo anaamini itamuimarisha kibiashara mwanamuziki huyo Barani Afrika.

Hii sio mara ya kwanza kwa msanii huyo kuzuru Uganda, mwezi Aprili mwaka huu alifanya mkutano mwingine wa kibiashara na rais Museveni.

Akon alitua nchini humo Aprili 2 ambapo alilakiwa na mmoja wa washauri wa Rais Museveni na ambaye pia ni mwanamuziki nyota wa Uganda, Eddy Kenzo.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Jumatatu, Mei 17, Rais huyo alisema alifanikisha mkutano wa kibiashara kati yake na wawekezaji hao.

Akifanya matani, Rais Museveni alimpea mkewe Akon jina la Kiganda Ihangwe.

" Leo nilikutana na mwanamuziki ambaye ni mzaliwa wa Senegal lakini pia ni raia wa Marekani Aliaune Badara Akon pamoja na mkewe katika ikulu ya Entebbe kujadili masuala ya kibiashara," Museveni alisema.

Akon pia alikuwa ajadili na Rais Museveni kuhusu masuala ya utalii, kawi na maendeleo mengine ya miundombinu.

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke