Mahakama nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imemuachia huru aliyekuwa mkuu wa wafanyakazi wa Rais Félix Tshisekedi kwa tuhuma za rushwa, kwa mujibu wa wakili wake.
Vital Kamerhe alihukumiwa mwaka wa 2020 hadi miaka 20 ya kazi ngumu baada ya kukabiliwa na mashtaka ya ubadhirifu wa karibu $50m (£39m) ya fedha za umma.
Pesa zilizotoweka zilikusudiwa kutumika katika mradi wa ujenzi wa nyumba uliotangazwa na rais baada ya kuapishwa kwake.
Kuachiliwa kwake na Mahakama ya Rufaa katika mji mkuu, Kinshasa, kuliwasilishwa kwa mawakili wa Bw Kamerhe, kulingana na mashirika ya habari.
Ilitaja ukosefu wa ushahidi na kumwondolea mashtaka yote.
Bw Kamerhe alikuwa mtu mashuhuri zaidi kuhukumiwa kwa ufisadi nchini DR Congo.
Lakini wakili wake, Hugues Pulusi, aliwaambia waandishi wa habari siku ya Alhamisi kwamba "haki imerekebisha udhalimu wake".
Mahakama ya awali ya rufaa ilipunguza kifungo chake cha miaka 20 hadi miaka 13, kabla ya kuachiliwa huru siku ya Alhamisi.