Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mrembo mwenye miaka 25 ajifungua pacha tisa

9b4d3a5cecec72b8 Mrembo mwenye miaka 25 ajifungua pacha tisa

Wed, 5 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Wizara ya Afya ya Mali ilifichua kwamba Halima Cisse alijifungua wasichana watano na wavulana wanne kupitia njia ya upasuaji

- Mama huyo mwenye miaka 25, amekuwa chini ya uangalifu wa madaktari jijini Bamako kwa wiki mbili lakini alihamishwa hadi Morocco kwa matibabu spesheli baada ya amri ya Rais Bah Ndaw

- Wanamtandao waliduwazwa na taarifa hiyo wengi wakisema ni baraka kubwa Afrika

Mwanamke mmoja mwenye miaka 25, nchini Mali amejifungua watoto tisa na kuweka historia ya kuwa mmoja wa wanawake duniani kuzaa pacha tisa.

Kulingana na Wizara ya Afya ya Mali, mama huyo aliyetambuliwa kama Halima Cisse alikuwa anatazamiwa kuzaa watoto saba lakini uchunguzi wa ultrasound haukutambua kwamba alikuwa na watoto wengine wawili zaidi tumboni.

Wizara hiyo ilifichua kuwa Cisse alijifungua wasichana watano na wavulana wanne kupitia njia ya upasuaji.

Halima amekuwa chini ya uangalifu wa madaktari jijini Bamako kwa wiki mbili lakini alihamishwa hadi Morocco kwa matibabu spesheli baada ya amri ya Rais Bah Ndaw.

Waziri wa Afya wa Mali, Fanta Siby alisema mama huyo an malaika wake wanaendela vizuri na wataruhusiwa kwenda wiki chache zijazo.

Wanamtandao waliduwazwa na taarifa hiyo wengi wakisema ni baraka kubwa Afrika.

Hii hapa maoni yao:Philip McCloude alisema: "Mama wa Mali azaa watoto tisa! Baraka ilioje Afrika."

Tana Poindexter aliandika: "Watoto tisa, hii ni maajabu tu kwa mara ya kwanza."

Katika taarifa sawia na hiyo, TUKO.co.ke iliripotia kuhusu mama mmoja Kisii ambaye alizaa watoto watano.

Sheila Nyanchera, alijifungua kwa mara ya kwanza pacha watano Alhamisi, Aprili 15, na kumuwacha mume wake akiwa amejaa furaha na pia wasiwasi.

Mume wa Nyanchera, Douglas Nyaoko, alisema ndoto tyake ilikuwa kuwa padri wa Kanisa Katoliki lakini mambo yaligeuka alipokutana na mke wake.Wawili hao wameoana kwa miaka miwili.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke