Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mrembo amng'oa polisi sikio usiku na habari zingine za kusisimua wiki hii

160174fd2b9bda0b Mrembo amng'oa polisi sikio usiku na habari zingine za kusisimua wiki hii

Thu, 8 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kila siku ya wiki, TUKO.co.ke inakupakulia kwa mukhtasari matukio na habari muhimu zilizogonga vichwa vya habari wiki hii ili ukapate kufahamu kwa upana na utendeti mambo yalivyo ulimwenguni.

1. Mrembo Amshambulia Polisi, Ampiga na Kumng'oa Sikio Wakati wa Kafyu

Afisa wa polisi anauguza majereha mabaya baada ya mwanamke mmoja mkazi wa Nairobi kumuuma sikio lake hadi kuling'oa wakati wa saa za kafyu.

Mrembo huyo alimrukia afisa wa polisi na kumshika kichwa chake kwa nguvu na kumuuma sikio hadi kuling'oa.

Wakati huo huo Afisa wa KDF Aaga Dunia Baada ya Mpenzi wake Kumuuma Kahawa Wendani

Mrembo aliyetambuliwa kwa jina kama Violet Asala anazuiliwa na maafisa wa upelelezi baada ya kumuua mpenzi wake.

Kulingana na Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Violet alimuuma mpenzi wake mara kadhaa na kumfanya kupoteza fahamu.

Asala ni mwanamuziki chipukizi ambaye anapenda kuchapisha picha za shughuli zake kwenye Instagram.

3. Video ya Mahaba ya Mwanamuziki Samidoh na Karen Nyamu Yawaduwaza Wanamitandao

Video ya mwanasisasa Karen Nyamu na baba wa mtoto wake mwanamuziki Samidoh ilizua hisia mseto miongoni mwa Wakenya.

4. COVID-19: Uingereza Yasitisha Safari za Ndege Kutoka Kenya

Ubalozi wa Uingereza humu nchini ulisitisha safari za ndege kwa abiria wanaotoka Kenya kwa ajili ya idadi kubwa ya maambukizi ya COVID-19.

Ubalozi huo ulisema kwamba masharti hayo yataanza kuzingatiwa Ijumaa, Aprili 9.

Kenya ilijibu uamuzi huo huku Shirika la Ndege la Kenya(KQ), likisitisha safari za ndege kutoka na kuelekea Uingereza kufuatia agizo la serikali.



5. Polisi Watibua Kikao cha TangaTanga na Wanahabari Hotelini Kuhusu Mkopo wa IMF

Haya yanajiri huku wakenya mitandaoni wakizidi kupinga uamuzi wa taifa kukopa KSh 267.6 bilioni.

Wakionyesha ghadhabu yao, wananchi wamezidi kupinga mpango wa serikali ya Jubilee kupewa mkopo tangu siku ya Ijumaa, Aprili 2, 2021.



Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke