- Zian Achana alipakia picha zake mitandaoni wiki chache baada ya kukamatwa kuhusiana na madai ya mauaji
- Muimbaji huyo alikuwa amevaa rinda la manjano, kujipodia na kuonyesha mapozi
- Mshukiwa huyo wa uhalifu aliambatanisha jumbe kadhaa kwenye picha zake akisema namna Mungu alimpigania
Muimbaji Mkenya aliyetuhumiwa kumuua mume wake ambaye alikuwa afisa wa KDF, amerejea mitandaoni kwa kishindo baada ya kuwa kimya wiki kadhaa.
Zian Achana ambaye jijna lake la kuzaliwa ni Volet Asale, alikamatwa wiki chache zilizopita baada ya kudaiwa kumuuma mume wake Daniel Omollo Onyango, hadi kumuua.
Mnamo Jumanne, Mei 4, msanii huyo alipakia picha zake mitandaoni akiwa amevaa rinda la manjano na viatu maridadi vya visigino.
Alikuwa ameachilia nywele zake ndefu na pia kuchapisha picha zake akiwa na binti yake.
Mshukiwa huyo wa uhalifu aliambatanisha jumbe kadhaa kwenye picha zake akisema namna Mungu alimpigania.
Alisema: "Si rahisi kama munavyofikiria. Imani yangu na Mungu itanisimamia.Mungu atakupigania kila wakati. Maneno ya busara ya familia."
Haijabanika wazi endapo Achana ameachiliwa kwa dhamana wala sababu za kuachiliwa kwake kutolewa.
Mshukiwa wa mauajiAchana ambaye ni mwanamuziki chipukizi, anaripotiwa alikuwa anapanga kuhamia Kasarani na kumkera mume wake ambaye hakufurahishwa na hatua hiyo.
Kulingana na Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Violet alimuuma mpenzi wake mara kadhaa na kumfanya kupoteza fahamu.
Alipogundua kwamba mambo yamezidi unga, alijaribu kumkimbisha katika kituo cha matibabu cha Kahawa Garrison ambapo alithibitishwa kufariki alipowasili.
READ ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.