Sun, 12 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mahakama nchini Benin imemhukumu mmoja wa Wapinzani wakuu wa Rais Patrice Talon kwa kuhusika katika vitendo vya ugaidi.
Reckya Madougou ambaye amewahi kuwa Waziri wa Sheria katika Serikali ya Rais Thomas Boni Yayi amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela.
Hukumu yake imekuja siku chache baada ya Mpinzani mwingine mkubwa wa Rais Talon, Joel Aivo kuhukumiwa miaka 10 kwa tuhuma za kupanga njama dhidi ya Serikali na utakatishaji Fedha.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live