Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mpiga picha wa DP Ruto amwandikia ujumbe mtamu: "Umenitoa Mbali"

4c47ee5ed777f687 Mpiga picha wa DP Ruto amwandikia ujumbe mtamu: "Umenitoa Mbali"

Fri, 18 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mpiga picha aliyetambuliwa kama Mwangi, alichapisha ujumbe mitandaoni kumshukuru William Ruto kwa nafasi ya kazi aliyompaMwangi alisema alikuwa mpiga picha tu kutoka kijijini asiyekuwa na tumaini maishani lakini Ruto amependua maisha yake na kuyaboreshaMwanahabari huyo hapo awali alifanya kazi Ikulu na vile vile K24 kabla ya kuajiriwa naibu raisMpiga picha wake Naibu Rais William Ruto alichapisha ujumbe kwenye kurasa zake za mitandaoni kumshukuru DP kwa kumpa fursa ya kumfanyia kazi.

Mpiga picha huyo ambaye awali alifanya kazi na shirika la utangazaji la K24 na vile vile Ikulu alikuwa mpiga picha chipukizi asiyekuwa na tumaini maishani lakini Ruto alibadilisha maisha yake.

Kwenye ujume aliouchapisha Facebook, Alhamisi, Juni 17, mwanahabari huyo kwa jina Mwangi alimshukuru Ruto sio tu kwa kumpa fursa ya kufanya kazi naye bali pia kumuamini yeye na wenzake.

"Nilikuwa mpiga picha wa kijiji bila tumaini, sikuwa na uhakika wa maisha yangu ya mbeleni lakini umenifanya kuwa mtu wa maana leo. Kutoka mioyoni mwetu, Dkt William Samoei Ruto (WSR) Naibu Rais wa Kenya, asante sana kwa kutuamini na pia kutupa fursa ya kufanya kazi nawe. Mimi na wenzangu," alisema.

Awali, Mwangi alifanya kazi na K24 akapanda hadhi hadi akawa mpiga picha wa Ruto.

Kwenye taarifa nyingine, TUKO.co.ke ilimshukuru Mkenya anayefanya kazi katika benki Dubai ambayo alijitolea kurejea nchini kumfanyia kampeni naibu rais katika azma yake ya kuingia Ikulu 2022.

Dada huyo kwa jina Hellen alichapisha ujumbe kwenye Twitter kudhihirisha penzi lake kwa naibu rais na kubainisha kwamba yuko tayari kujitolea kuwa agenti wa Ruto bila malipo.

Akimjibu ujumbe wake, DP alimshukuru dada huyo, ambaye kulingana na wasifu wake kwenye Twitter anafanya kazi kama afisa wa mkopo Islam Bank kule Dubai.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke