Fri, 28 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Serikali ya Rwanda imeridhia kufungua tena mpaka wake na Uganda uliofungwa kwa muda wa miaka mitatu kufuatia madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanyika kwa raia wa Rwanda waishio nchini Uganda.
Katika kipindi hichohicho Rwanda iliishutumu Uganda kuongoza makundi yaliyokuwa yakipinga uongozi wa Rais Kagame nchini Rwanda
Mpaka huo unatarajiwa kufunguliwa tarehe 31, Januari mwaka 2022 wakati nchi zote mbili zikiendelea kujadili masuala kadhaa yaliyochochea adha hiyo ili kufikia muafaka.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live