Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Moses Kuria atofautiana na uamuzi wa Kiraitu kujipenda baada ya kupona COVID-19

607969b1019abbef Moses Kuria atofautiana na uamuzi wa Kiraitu kujipenda baada ya kupona COVID-19

Tue, 27 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mbunge Moses Kuria alitofautiana na mawazo ya busara ambayo Gavana wa Meru Murungi aliyatoa baada ya kupona kutoka kwa COVID-19

- Kuria alisema gavana huyo ana jukumu kubwa alilopewa na Mungu zaidi ya kulenga familia yake tu

- Baada ya kupona virusi alisema alikuwa ametambua jinsi COVID-19 ilivyomnyang'anya maisha yake, sauti na mawazo

Mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria amemkosoa Gavana wa Meru Kiraitu Murungi kwa wazo lake la kujipenda na kuyalinda maisha yake binafsi na familia yake baada ya kupona COVID-19.

Murungi alisema kuwa hali ya kujitenga alipokuwa mgonjwa kumemfanya atafakari juu ya jinsi siasa zilivyompokonya maisha yake, na hivyo basi atapuuza kelele za siasa na badala yake kufuata kile nafsi yake inapendelea.

Kuria alisema wazo la gavana lilikuwa la ubinafsi akiongeza kuwa ana jukumu kubwa zaidi alilopewa na Mungu zaidi ya kutumikia familia yake ya karibu.

"Nadhani ikiwa Mungu atakuokoa kutoka kwa hali mbaya kama hii wakati wengine hawana bahati na wanapoteza maisha, ana kusudi kubwa kwako kuliko wewe mwenyewe au familia yako ya karibu," mbunge huyo alisema.

Mbunge huyo wa Tanga Tanga alisema Murungi alinapswa kuwatumikia watu wake kwa bidii zaidi ya kuwa mbinafsi.

"Nimesikitishwa na ubinafsi wa Gavana Kiraitu. Hapana Bwana Gavana, Mungu alituokoa ili tuwahudumie watu hata zaidi," Kuria alisema.

Murungi alipimwa na kupatikana na COVID-19 Machi 2021 na wakati akikabiliana na maradhi hayo alipitia nyakati ngmu zilizomfanya apoate funzo kwamba maisha ni muhimu zaidi kuliko siasa.

"Safari ya coronavirus ilinipa nafasi ya kutafakari safari yangu ya kisiasa. Laiti ningekufa, ningekuwa peke yangu na kelele na zogo la siasa lingeendelea bila mimi," gavana alisema.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke