Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Moses Karua aachiliwa baada ya kukamatwa awali kwa kukaidi maagizo ya COVID-19

Ae7d344f934065dd Moses Karua aachiliwa baada ya kukamatwa awali kwa kukaidi maagizo ya COVID-19

Tue, 13 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mahakama iliamuru mwanasiasa huyo kulipa KSh 750,000 faini au kutumikia kifungo cha miezi minane gerezani

- Kuria ambaye alichapisha ujumbe kwenye Facebook mnamo Jumanne, Aprili 13 akieleza yaliyomfika alikosa kutaja sababu za kukamatwa kwake

- Seikali ilipiga marufuku kwa mikutano ya hadhara na kuamuru maeneo ya maankuli kuuza chakula kwa wateja wa kununua na kuondooka ili kudhibiti maambukizi ya COVID-19

Mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria ameachiliwa na mahakama ya Kiambaa baada kukamatwa akiwa na wenzake 30 kwa kukiuka maagizo ya Wizara ya Afya kudhibiti COVID-19.

Mahakama iliamuru mwanasiasa huyo kulipa KSh 750,000 faini au kutumikia kifungo cha miezi minane gerezani.

Kuria alikutwa na hatia ya kutovalia maski, kuzurura nje nyakati za usiku na vile vile kuandaa mkutano wa hadhara.

Kuria ambaye alichapisha ujumbe kwenye Facebook mnamo Jumanne, Aprili 13 akieleza yaliyomfika alikosa kutaja sababu za kukamatwa kwake.

Hata hivyo alipakia picha akiwa kizimbani bila maski.

Wakati wa hotuba yake ya 15 kwa taifa, Rais Uhuru Kenyatta alitangaza kufunga kwa kaunti za Nairobi, Kajiado, Machakos, Kiambu na Nakuru maeneo yaliyoathirika na virusi vya corona kwa asilimia 75.

Wakati uo huo aliamuru kuwa hakuna kutoka wala kuingia katika sehemu hizo kwa njia yoyote ile.

Hata hivyo baadhi ya Wakenya wamekuwa wakikaidi amri hiyo na kuandaa mikitano ya hadhara.

Mnamo Jumatatu, Aprili 12 Wizara ya Afya iliripoti watu 486 walinasa virusi vya corona kutokana na sampuli 2,989 zilizopimwa.

Asilimia ya maambukizi Kenya imefika 16.3.

Kufikia sasa idadi ya wagonjwa wa virusi vya COVID-19 imetimia 146,156 kutokana na sampuli 1,564,287 kupimwa.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke