Tue, 26 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Familia zaidi ya milioni moja zinatarajiwa kunufaika na mpango mpya wa nchi ya Morocco wa kuanza kuzilipa kaya maskini kwa kila mwezi.
Tovuti ya DW imeripoti kuwa familia hizo zitapata kuanzia dirham 500 ambayo ni sawa na Sh126,000 kwa mwezi.
Waziri Mkuu wa Morocco, Aziz Akhannouch amesema malipo hayo yataanza Alhamisi ya Desemba 29, 2023. Mpango huo ni utekelezaji wa ahadi ya kiongozi mkuu wan chi hiyo, Mfalme Mohammed VI.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live