Tue, 12 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Idadi ya waliofariki tetemeko la ardhi Morocco wamefikia 2,800.
Madaktari na waokoaji wanaendelea kupambana huku matumaini yakififia kupata watu wakiwa hai ambao wanadhaniwa kufukiwa chini ya vifusi kutokana na miundombinu.
Umoja wa Mataifa umesema kwamba takriban watoto 100,000 wameathiriwa na tetemeko hilo.
Waokoaji kutoka nchi za Qatar, Uhispania, Falme za Kiarabu na Uingereza wamejitolea katika shughuli za utafutaji na uokoaji unaendelea nchini humo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live