Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mombasa: Rais Uhuru Kenyatta, Raila Odinga wakutana na viongozi wa OKA

57ff351b196ad310 Mombasa: Rais Uhuru Kenyatta, Raila Odinga wakutana na viongozi wa OKA

Tue, 10 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kulingana na taarifa kutoka Ikulu mnamo Jumanne, Agosti 8, mkutano huo uliandaliwa kujadili masuala yanayolikumba taifaViongozi waliokuwepo katika kikao hicho ni Raila Odinga (ODM), Kalonzo Musyoka (Wiper) Musalia Mudavadi (ANC), Moses Wetangula (Fore Kenya) na Gideon Moi (Kanu) Mkutano wa Mombasa unajiri wakati Naibu Rais William Ruto na kikosi chake wamesuta vikali handisheki wakisema imelemaza uchumi wa taifaRais Uhuru Kenyatta alifanya kikao na Kinara wa ODM Raila Odinga na Viongozi wa Muungano wa OKA Kalonzo Musyoka (Wiper) Musalia Mudavadi (ANC), Moses Wetangula (Fore Kenya) na Gideon Moi (Kanu) katika Ikulu ya Mombasa.

Kulingana na taarifa ya msemaji wa Ikulu Kanze Dena, Uhuru alikutana na viongozi hao ili kujadili maswala yanayolikabili taifa.

Vile vile Gavana wa Kakamega na ambaye pia ni naibu kiongozi wa chama cha Orange Democratic Movement Wycliffe Oparanya alikuwepo.

Miongoni mwa maswala yaliyojadiliwa na viongozi hao ni athari za COVID-19 kwa taifa na jinsi ya kufufua uchumi kando umuhimu wa kudumisha amani, umoja na utangamano.



Read also

Magazeti Ijumaa Julai 6: DP Ruto Asema Atachomoka Kutoka Serikali Wakati Ukifika

Mkutano huo unajiri siku chache baada ya Mudavadi, Wetangula na Kalonzo kuondoka katika muungano wa National Super Alliance (NASA) wakilalamikia dhuluma na usaliti kutoka kwa ODM.

Rais amekuwa akijitahidi kuwaunganisha viongozi hao wakati Uchaguzi Mkuu wa 2022 unakaribia.

Mwezi jana, Uhuru alitangaza kwamba atamchagua mrithi wake 2022 kutoka kwa viongozi wa NASA iwapo wataungana na kuafikiana kumpa mmoja wao nafasi ya kuwania urais.

Uhuru aliwapa changamoto viongozi hao kuungana ili kuimarisha nafasi yao ya kuunda serikali wakati hatamu yake itakapokamilika.

Hii ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Uhuru kutangaza waziwazi jinsi atakavyomchagua mrithi wake hata wakati vigogo wa kisiasa wanabishana kila mmoja wao akitaka kuungwa mkono na kiongozi wa taifa.

Mkutano wa Mombasa unajiri wakati Naibu Rais William Ruto na kikosi chake wamesuta vikali salamu za maridhiano ambazo alisema zimelemaza uchumi wa taifa na Agenda Nne Kuu za serikali.

Katika taarifa yao ya Alhamisi, Agosti 5 baada ya mkutano wa Wabunge cha 'Hustlers' huko Karen, wanasiasa hao walisema kwa sababu hiyo, Agenda Nne Kuu za Afya kwa Wote, Makazi Bora, Ukuaji wa Viwanda na Utoshelezo wa Chakula zimelemazwa.



"La kusikitisha ni kwamba muungano wa Nasa, vinara wake na baadhi ya washirika wa Jubilee wameiteka nyara serikali na agenda zake zote kuu," mbunge wa Kandara Alice Wahome ambaye alisoma sehemu ya taarifa hiyo alisema.

"Waliendesha vibaya uchumi na kusababisha kuongezeka kwa deni kwa kiasi kikubwa ambacho kimelifinya taifa."

Wabunge hao walisema mara kwa mara wamekuwa wakiteta kuhusiana na jinsi Jubilee ilivyopuuza agenda zake ambazo iliahidi kuwatimizia wananchi wakati wa uchaguzi wa 2017.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke