Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Molo: Mtahiniwa wa KCSE Apatikana Ameaga Dunia

A0c8327a1b4a9134 Molo: Mtahiniwa wa KCSE Apatikana Ameaga Dunia

Wed, 24 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mtahiniwa wa darasa la 8 mwenye umri wa miaka 14 aliaga dunia baada ya kuteleza na kuanguka kwenye daraja la reli katika eneo la Michina, kaunti ndogo ya Molo.

Naibu Chifu wa neo hilo Kennedy Kiago alithibitisha kisa hicho cha kusikitisha ambacho kilisababisha kifo cha mtoto huyo mwenye umri mdogo.

Kulingana na ripoti ya Citizen TV Kiago alisema kuwa marehemu, aliyejulikana kama Beatrice Gesare alikumbana na mauti akiwa njiani kuelekea dukani.

Gesare, binti wa pekee katika familia yake alikuwa pekee yake wakati wa tukio hilo na iliwachukua wazaziwe muda mrefu kubaini kilichokuwa yametokea kwa muda ufaao.

Mwanzoni, aliripotiwa kutoweka Jumapili hadi jana wakati wakazi wa eneo hilo walipoupata mwili wake mita 30 ardhini kutoka kwenye daraja hilo.

Kulingana na wazaziwe, Gesare alikuwa ametumwa dukani baada ya kutoka kanisani katika ambapo alitoweka mchana huo na juhudi za kumtafuta zikaambulia patupu.

Babake, David Nyaminja, alimtaja mwanawe kama mwenye furaha na mchapakazi. Aliongeza kuwa ndoto yake ya kuwa mwalimu ilikatizwa ghafla kutokana na kifo chake.

Wenyeji waliitaka serikali ya kaunti kuwajibika na kukarabati daraja hilo ambalo walisema limesababisha vifo vya watu watatu huku wengine kadhaa wakijeruhiwa.

Kwingineko, mnamo Jumanne, Machi 23 mtahiniwa wa KCPE kutoka Shule ya Msingi Pesi katika Kaunti ya Nyandarua alifariki dunia muda mfupi baada ya kujifungua.

Ripoti za polisi zilionesha kwamba alianza kuumwa dakika chache kabla ya kuukalia mtihani wa somo la Sayansi saa 8.30 asubuhi.

Alipelekwa katika zahanati ya Pesi ambapo baada ya kujifungua alikumbwa na matatizo ya kiafya na kusafirishwa hadi hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Nyahururu alipofariki dunia muda mfupi baada ya kulazwa.

Mwili wa mwendazake sasa umehifadhiwa katika mochuari ya hospitali ya Nyahururu ukisubiri kufanyiwa upasuaji.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke