Tue, 6 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Washukiwa wanne wa kesi ya mlipuko wa gesi Embakasi wamefikishwa mahakamani Jumanne.
Katika maombi mbalimbali, Kurugenzi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) ilitaka washukiwa; Derrick Kimathi, Joseph Makau, David Walunya Ong'are na Marrian Mutete Kioko wawekwe mahabusu ili kukamilisha uchunguzi dhidi yao.
Kimathi ndiye mmiliki wa kiwanda cha kujaza gesi eneo la Embakasi jijini Nairobi ambako moto ulizuka Alhamisi usiku na kuua watu sita na kuwajeruhi karibu wengine 300.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live