Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkuu wa utawala wa kijeshi wa Mali ajadiliana na Rais wa Urusi

Mali Rusia Putin Mkuu wa utawala wa kijeshi wa Mali ajadiliana na Rais wa Urusi

Wed, 11 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Rais wa mpito wa Mali na rais wa Urusi Vladimir Putin wamejadili ushirikiano wa kiuchumi na kiusalama wakati wa mazungumzo ya simu.

“Wakati wa majadiliano ya simu, nilizungumza na Rais Putin kuhusu ushirikiano wetu katika nyanja za kiuchumi, usalama na kukabiliana na ugaidi. Nilitoa shukrani zangu kwa msaada wote ambao Urusi inaipa Mali,” Kanali wa Mali Assimi Goita alisema katika taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wa X uliokuwa ukijulikana zamani kama Twitter.

Hayo yameungwa mkono na Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi.

Katika taarifa yake kwenye Telegram, ilisema viongozi hao wawili "walithibitisha dhamira yao ya pamoja ya kuimarisha zaidi uhusiano wa kibiashara na kiuchumi, ushirikiano katika kutoa usalama, na kupambana na ugaidi.Upande wa Mali ulitoa shukrani zake kwa misaada mbalimbali inayotolewa na Urusi".

Haya ni mazungumzo ya tatu kwa simu kati ya viongozi hao wawili katika muda wa miezi kadhaa.

Mamluki wa Urusi kutoka Kundi la Wagner wanachukua nafasi kubwa katika mashambulizi yanayoendelea ya jeshi la Mali dhidi ya waasi wa zamani wa Tuareg katika mji wa Kidal, ikiwa ni pamoja na kuuteka mji wa kimkakati wa Anefis tarehe 6 Oktoba baada ya siku kadhaa za mapigano makali.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live