Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkuu wa Upelelezi ahukumiwa kifo

Kifo Ahukumiwa Mkuu wa Upelelezi ahukumiwa kifo

Thu, 14 Jul 2022 Chanzo: BBC

Jaji mmoja nchini Gambia amemhukumu kifo aliyekuwa mkuu wa upelelezi wa nchi hiyo, Yankuba Badjie, na maafisa wengine wanne wa usalama kwa mauaji ya mwaka 2016 ya mwanaharakati wa kisiasa katika siku za mwisho za utawala wa kikatili chini ya Rais wa zamani Yahya Jammeh.

Mwanaharakati, Ebrima Solo Sandeng - kiongozi mkuu katika chama cha upinzani cha United Democratic Party - alikuwa amekamatwa wakati wa maandamano ya kuipinga serikali.

Alikufa gerezani siku mbili baadaye, baada ya kupigwa na kuteswa.

Kifo chake kilichochea wimbi la hasira ya wananchi ambayo hatimaye ilisababisha kuondolewa madarakani kwa Rais Jammeh baada ya miaka 22 madarakani.

Bw Jammeh alikimbia mwaka wa 2017 hadi Equatorial Guinea, ambako bado yuko uhamishoni.

Chanzo: BBC