Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkuu wa Kupambana na Rushwa asimamsihwa kazi kwa tuhuma za Ufisadi

Rushwa SA.jpeg Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa na Busisiwe Mkhwebane

Sat, 11 Jun 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amemsimamisha kazi Mkuu wa Kitengo cha Kupambana na Ufisadi kwa shutuma za upendeleo wa kisiasa.

Wakili Busisiwe Mkhwebane anadaiwa kutawaliwa na shutuma za upendeleo wa kisiasa ambapo idadi kubwa ya uchunguzi wake toka ateuliwe mnamo 2016, umekataliwa na Mahakama, na hivyo kuzua maswali kuhusu kustahili kwake kushika wadhifa huo.

Aidha, Juni 8, 2022, Mkhwebane alisema amepokea malalamiko dhidi ya Ramaphosa ya kukiuka maadili ya kiutendaji

Taarifa iliyotolewa na msemaji wa Rais Ramaphosa inasema kuwa kutokuwepo kwa Wakili huyo ofisini "hakutazuia maendeleo ya uchunguzi wowote unaosubiri au unaoendelea" na kwamba atasimamishwa kazi hadi mchakato wa kumuondoa ukamilishwe na bunge.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live