Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkurugenzi wa Equity motoni kuhusu Ksh. Bilioni 15 alizopewa rafiki wa Ruto

77e1d02fc70d9479 Mkuu wa Equity motoni kuhusu KSh15B zilizopewa rafiki Mturuki wa Ruto

Sun, 22 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Afisa Mkuu Mtendaji wa Benki ya Equity, James Mwangi atafika mbele ya Kamati ya Bunge nchini Kenya siku ya Jumatano, Agosti 25. Mwangi anatazamiwa kujibu maswali saba kuhusu namna swahiba Mturuki wa Naibu Rais William Ruto alipokea mkopo wa KSh 15 bilioni kutoka kwa benki hiyo.

Ruto alifichua kuwa Harun alipokea pesa hizo ili kujenga kiwanda cha kutengeneza chanjo nchini Uganda Afisa Mkuu Mtendaji wa Benki ya Equity, James Mwangi ameagizwa kufika mbele ya Kamati ya Bunge la Kitaifa kuelezea kinaga ubaga namna swahiba Mturuki wa Naibu Rais William Ruto, Aydin Harun alipokea KSh 15 bilioni kutoka kwa benki hiyo.

Harun aligonga vichwa ya habari wiki chache zilizopita baada ya Ruto kuzuiwa kusafiri hadi nchini Uganda kwa kutokuwa na kibali kisha baadaye Mturuki huyo alitimuliwa nchini kwa madai ya kuhusika katika visa vya kigaidi.

Kwa mujibu wa ripoti ya Daily Nation, kamati ya Bunge kuhusu Fedha inamtaka Mwangi kujibu maswali saba kuhusu namna Harun alipata pesa hizo kutoka kwa benki hiyo



Ruto alikuwa amefichua kwamba Harun alipokea pesa hizo ili kujenga kiwanda cha kutengeneza chanjo nchini Uganda

Mwanzo, Mwangi anatakiwa kuweka bayana iwapo benki hiyo ilifuata sheria na masharti kabla ya kutoa pesa hizo.

Fauka ya hayo, kamati hiyo inayoongozwa na Gladys Wanga pia inataka kujua iwapo benki hiyo ilimfanyia uchunguzi wa kina Mturuki huyo kisheria.

Mwangi pia anatakiwa kufafanuwa iwapo benki yake ilifuata sheria sehemu ya 43 kuhusu Uhalifi na Utapeli wa Pesa ambayo huzitaka benki kutafuta taarifa kamili kumhusu mteja wao kabla kufanya biashara nao.

Mkutano huo utafanyika Jumatano, Agosti 25, katika majengo ya bunge.

Aydin Harun afukuzwa KenyaKama ilivyoripotiwa awali, Harun ambaye alikuwa chanzo cha kutibuka kwa ziara ya Ruto nchini Uganda, alitimuliwa nchini Jumatatu, Agosti 9.

Mfanyabiashara huyo anaripotiwa kupandishwa kwenye ndege ya shirika la Uturuki mwendo wa saa kumi na moja asubuhi na kutua jijini Istanbul ambapo alipokelewa na maafisa wa usalama ili kuhojiwa zaidi.



Aydin alikuwa kati ya waliozuiwa kusafiri hadi Uganda akitokea Kenya pamoja na Ruto mnamo Jumatatu, Agosti 2.

Kisha maafisa wa uhamiaji katika Uwanja wa Ndege wa Wilson walimchukuwa ili kumhoji punde alipotua akitokea Uganda.

Baadaye Wizara ya Usalama wa Ndani ulisema serikali ilimtimua kwa sababu ya kuhusika katika utakatishaji fedha haramu na ombi la maafisa wa usalama jijini Instabul.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke