Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkewe Marehemu Rais Robert Mugabe amelazwa hospitalini Singapore

841667611521ad6c Mkewe Marehemu Rais Robert Mugabe amelazwa hospitalini Singapore

Wed, 19 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Binamu wa mke wa marehemu Rais Robert Mugabe amefichua kwamba Mama Grace Mugabe ni mgonjwa na amelazwa katika hospitali moja nchini Singapore

- Mama Grace alitakiwa kufika mbele ya kamati inayomkashifu kwa kuandaa mazishi ya mumewe kinyume na tamaduni

- Zhuwawo alisema shangazi yake amekuwanchini humo kwa muda kaipokea matibabu

Mke wa marehemu Rais Robert Mugabe amelazwa katika hospitali moja nchini Singapore ambapo amekuwa akipokea matibabu kwa majuma kadhaa sasa.

Habari hizo zilitangazwa na binamuye Patrick Zhuwawo ambaye aliikashifu serikali ya Zimbabwe kwa kuikadamiza na kuifuatilia sana kisiasa familia ya Mugabe.

Akiwa kwenye mahojiano na televisheni moja nchini Afrika Kusini Jumatano Mei 12, Zhuwawo alisema shangazi yake hangeweza kufika kwenye kikao hicho kwa sababu za kiafya na hakuwa nchini kwa wakati huo.

" Anafahamu vema kwamba Amai Mugabe ni mgonjwa na hayupo nchini kwa sababu za kiafya, anajua kwamba anapokea matibabu nchini Singerpore, sijui ni kwa nini ameichukulia sana masuala ya kisiasa kuwa kikwazo kwa familia ya Mugabe," Alisema Zhuwawo.

Kulingana na Zhuwawo, waziri huyo wa zamani na ambaye yuko uhamishoni Afrika Kusini, alisema shangazi yake atahudhuria vikao hivyo atakapopata nafuu.

Hata hiyo, alimtuma mmoja wa maafisa wake kumwakilisha kwenye kesi anayokashifiwa kwa kumzika mumewe kinyume na tamaduni.

Mahakama ya kitamaduni imekuwa ikimshiniza Mama Amai kuidhinisha mwili wa mumewe kufukuliwa ili uzikwe kulingana na tamaduni lakini amekuwa akipuuzilia mbali mapendekezo hayo.

Mugabe alifariki dunia mwaka wa 2019 akipokea matibabu katika hospitali moja akiwa na umri wa miaka 95, hii ilikuwa miaka miwili baada ya kutimuliwa mamlakani ma wanajeshi.

Marehemu Mugabe alitawala Zimbabwe kwa miaka 37 na alizikwa nyumbani kwake Zvimba kilomita chache kutoka mji mkuu wa Harare.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke