Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkenya aliyekuwa akikwea Mlima Everest amefariki dunia

Mkenya Aliyekuwa Akiukwea Mlima Everest Cheruiyot Kirui Amefariki Dunia Mkenya aliyekuwa akiukwea Mlima Everest Cheruiyot Kirui amefariki dunia

Thu, 23 May 2024 Chanzo: Voa

Kulingana na gazeti la Himalayan Times mwili wa Bwana Kirui ulipatikana mita chache chini ya kilele cha Mlima Everest.

"Nia yake thabiti na shauku yake ya kupanda milima itakuwa msukumo milele. Tunatuma rambirambi zetu za dhati kwa familia na marafiki zake wakati huu wa majonzi."

Cheruiyot alikuwa kwenye misheni ya kuthubutu kufika kilele cha Mt Everest, bila oksijeni ya ziada.

"Aliandamana na mpanda mlima wa Nepal Nawang Sherpa, ambaye hatima yake bado haijulikani."

Cheruiyot alikuwa mfanyakazi wa benki na alikuwa amepanda hadi kilele cha Mlima Kenya, mara 15. Kupanda mlima Everest inahitaji uzoefu mwingi katika kupanda milima mahali pengine, cheti cha afya bora, vifaa na mwongozaji wa Kinepali mwenye uzoefu.

Theluji na barafu kwenye mlima husababisha hatari mbaya, kama vile maporomoko ya theluji, na kuna msimu kidogo wa kupanda kutokana na hali mbaya ya hewa.

Kwa urefu wa mita 8,849, kilele cha mlima Everest una takriban theluthi moja ya shinikizo la hewa ambalo lipo kwenye usawa wa bahari.

Chanzo: Voa