Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkenya Patrick Amoth ateuliwa kuwa rais wa bodi kuu ya WHO huko Geneva

731f5de1f4a9eab3.png Mkenya Patrick Amoth ateuliwa kuwa rais wa bodi kuu ya WHO huko Geneva

Thu, 3 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Patrick Amoth alichaguliwa wakati wa kikao cha 149 cha bodi kuu ya WHO kilichofanyika Jumatano, Juni 2

- Atachukua nafasi ya Waziri wa Afya wa India Harsh Vardhan, ambaye alichukua nafasi hiyo mnamo Mei 2020

- Amoth amekuwa kaimu mkurugenzi mkuu wa afya tangu Januari 2020 alipoteuliwa

Kaimu mkurugenzi mkuu wa Afya wa Kenya, Patrick Amoth, ndiye rais mpya wa Bodi Kuu ya Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO).

Amoth alichaguliwa wakati wa kikao cha 149 cha bodi kuu ya WHO kilichofanyika Jumatano, Juni 2.

Kufuatia uchaguzi huo, Amoth atachukua nafasi ya Waziri wa Afya wa India Harsh Vardhan, ambaye alichukua nafasi hiyo mnamo Mei 2020.

Kuchaguliwa kwa afisa huyo wa afya humu nchini kunampa madaraka zaidi baada ya kuwa makamu wa rais wa bodi kuu ya WHO mnamo tangu Mei 22, 2020.

Kikiwa chombo cha juu cha kufanya maamuzi katika shirika la afya, bodi kuu inaundwa na watu 34 waliohitimu kiufundi katika uwanja wa afya.

Kila mmoja anayeiwakilisha nchi mwanachama aliyechaguliwa kufanya hivyo na Bunge la Afya Ulimwenguni, hudumu kipindi cha miaka mitatu.

Bodi hufanya mikutano angalau mara mbili kwa mwaka, na wa kwanza utafanyika mnamo Januari mwaka ujao wakati ule mwingine umeitishwa mnamo Mei mara tu baada ya mkutano wa afya.

Baadhi ya majukumu muhimu ambayo timu mpya ya Amoth itashughulikia ni pamoja na lakini sio tu katika kutekeleza maamuzi na sera za mkutano, kuishauri, na kuwezesha kazi yake.

Amoth amekuwa akifanya kazi akiwa mkurugenzi mkuu wa afya tangu Januari 2020.

Safari ya AmothAmoth ana shahada ya udaktari na shahada ya Uzamili ya Tiba katika uzazi / magonjwa ya wanawake kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.

Alihudumu katika nafasi anuwai kuanzia afisa wa huduma za matibabu wa wilaya za Kiambu Mashariki na Magharibi kutoka 2001 hadi 2011.

Halafu alikua mtaalam mwandamizi wa matibabu katika uzazi / magonjwa ya wanawake katika hospitali ya wilaya ya Kiambu hadi Machi 2012.

Kisha alihamishiwa hadi Hospitali ya Machakos Level Five na kuwafanywa kuwa mtaalamu mkuu wa matibabu. Alishikilia nafasi hiyo hadi Oktoba 2013 alipopewa barua ya uhamisho hadi Hospitali ya Mama Lucy Kibaki katika nafsi hiyo hiyo na baadaye naibu mkurugenzi mwandamizi wa huduma za matibabu.

Kufuatia ugonjwa wa corona kufika nchini Kenya, Amoth alijitokeza hadharani kwa mara ya kwanza kabisa wakati wa kutano wa wandishi wa habari na Mawaziri wa Afya Mutahi Kagwe.

Wakati alipokuwa akijitokeza, majibu yake kwa maswali kutoka kwa wanahabari huwa yamejikita sana katika upande wa kiufundi kuhusiana na kuenea kwa virusi.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke