Fri, 13 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wakili wa mke wa Rais wa Gabon aliyeondolewa madarakani, Ali Bongo, anayefahamika kwa jina Sylvia Bongo amefungwa jela kufuatia mashtaka ya utakatishaji fedha, kupokea mali ya wizi na kughushi nyaraka.
Wakili Francois Zimeray amenukuliwa akisema Sylvia amefungwa kwa utaratibu usiyo halali.
Wakati hayo yanajiri mtoto wao, Noureddin Bongo Valentin pia amefunguliwa mashtaka ya rushwa, ubadhirifu wa fedha na kuwekwa kizuizini kabla ya kesi yake kuanza kusikilizwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live