Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mke amtema mumewe na kufanya harusi na "Roho Mtakatifu"

Ef7e35fbc2026e10 Mke amtema mumewe na kufanya harusi na "Roho Mtakatifu"

Thu, 27 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Elizabeth Nalem, mwenye umri wa miaka 41, ambaye ni afisa wa kaunti ya Pokot Magharibi aliandaa sherehe ya harusi yake na "roho mtakatifu" mjini Makutano

- Nalem alikuwa amevalia mavazi ya harusi huku shangwe na nderemo zikitanda hewani mume wake Joshua Nalem akimtazama kwa mshangao

- Mume wake ambaye wameishi pamoja kwa miaka 20 alisema alishangaa kumuona mke wake akila kiapo ya kumpenda 'mume mpya' asiyeonekana

Ukistaajbu ya Musa basi utayaona ya Firauni waliamba mababu.

Wakazi wa Pokot Magharibi walipigwa na butaa baada ya mwanamke mmoja kutangaza kuwa amefunga pingu za maisha na "roho mtakatifu".

Elizabeth Nalem, mwenye umri wa miaka 41, ambaye ni afisa wa kaunti ya Pokot Magharibi aliandaa sherehe ya harusi yake na "roho mtakatifu" katika hoteli ya Chelang'a, mjini Makutano.

Kwa mujibu wa gazeti la Taifa Leo, Alhamisi, 27, Nalem aliandamana pamoja na maafisa wenzake wa kaunti na wafanyabiashara wa kike katika karamu hiyo ambapo aliahidi kuwa mwaminifu kwa "mumewe" mpya.

Wakati wa hafla hiyo, Nalem alikuwa amevalia mavazi ya harusi huku shangwe na nderemo zikitanda hewani mume wake Joshua Nalem akimtazama kwa mshangao.

Karamu hiyo iliongozwa na Kasisi Albert Rumaita wa Kanisa la Full Gospel.

Kulingana na Nalem, amekuwa akitumikia dunia tangu kuzaliwa kwake lakini Roho Mtakatifu alimuaguza amtukie Mwenyezi Mungu.

"Nimetumikia dunia tangu nilipozaliwa. Lakini sasa Roho Mtakatifu ameniagiza nitumikie Mungu. Roho Mtakatifu alinituma kwa Pasta Rumaita ambaye alinunulia vazi la harusi, alianda hafla hii n akukodisha magari yaliyotuleta hapa," alisema.

Mume wake ambaye wameishi pamoja kwa miaka 20 alisema alishangaa kumuona mke wake akila kiapo ya kumpenda 'mume mpya' asiyeonekana.

Joshua Nalem alisema alitoa ng'ombe 22 na mbuzi 15 kama mahari alipomuoa mke wake lakini sasa amevunjika moyo kumuoana akiolewa na "mwanamume mwingine.

Mzee huyo alifichua kuwa ndoa yao ilainza kuyumba baada ya mke wake kubadilisha mtindo wake wa mombi akiamka usiku wa manane kuomba na kila alipoulizwa, alikuwa akitorea kwa jirani.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke