Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkasa wa ndege ya kijeshi: Maafisa 10 wa KDF waangamia na 13 kujeruhiwa

2d2e7cc454936a03 Mkasa wa ndege ya kijeshi: Maafisa 10 wa KDF waangamia na 13 kujeruhiwa

Fri, 25 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Ilikuwa asubuhi saa tatu wakati ndege hiyo ilipata matatizo ikiwa angani na kuanguka chini kama iliyodunguliwaMsemaji wa KDF alisema wataalamu wa masuala ya ajali za ndege wameanzisha uchunguzi ili kujua kilichosababisha ajali hiyoDuru zimearifu kuwa maafisa 10 walifariki papo hapo huku wengine wakiokolewa na kufikishwa hospitaliMaafisa 10 wa KDF wameripotiwa kuangamia katika mkasa wa ndege ya kijeshi uliotokea Alhamisi Juni 24 asubuhi katika eneo la Ngong kaunti ya Kajiado.

Naibu kamishna wa kaunti ya Kajiado Morang'a Morekwa alisema watu wengine 13 waliokuwa kwenye ndege hiyo walipata majeraha mabaya na kukimbizwa katika hospitali ya Defence Forces Memorial Hospital, Nairobi.

Ndege hiyo aina ya Mi-171E ilikuwa kwenye mafunzo wakati ambapo ilianguka asubuhi saa tatu katika eneo la Ol Tepesi.

Walioshuhudia mkasa huo walisema ndege hiyo ilionekana ikipoteza mwelekeo angani kabla ya kuanguka na kushika moto papo hapo.

“Leo asubuhi saa tatu ndege aina ya Mi 171e Air Force Helicopter, iliyokuwa kwenye shughuli za mafunzo ilianguka katika eneo la OlTepesi, Ngong, kaunti ya Kajiado," taarifa ya KDF ilisema.

Msemaji wa KDF Zipporah Kioko alisema wana rekodi ya wote waliokuwa kwenye ndege hiyo na tayari familia za walioangamia wamepata ripoti.

"Kwa bahati mbaya, kutokana na mkasa huo tumeweza kuwapoteza maafisa kadhaa. Tayari tumeanza kuwasiliana na familia zao ili kuwapa ujumbe na kutuma rambirambi za KDF," alisema Kioko.

Video iliyoibuka kutoka kwa walioshuhudia mkasa huo ilionyesha moshi mkubwa ukifuka baada ya ndege hiyo kuanguka.

Kikosi cha wataaamu wa ajali za ndege walitumwa katika eneo la mkasa ili kubaini kiini cha ndege hiyo kuanguka.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 073248269.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke