Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mjue Bernice Kariuki, Mkenya ambaye ni mpishi klabu ya Arsenal

1a692d0097cbdbfd Mjue Bernice Kariuki, Mkenya ambaye ni mpishi klabu ya Arsenal

Thu, 2 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Bernice Kariuki amekulia mtaani Jericho katika jiji la Nairobi Hata hivyo, alitia bidii na kujijengeya himaya yake ambapo sasa amepata nafasi ya kipekee ya kuwa mpishi wa klabu ya Arsenal. Ana uzoefu katika sekta ya hoteli na amewahi kuhudumu katika mahoteli ya kifahari nchini Uingereza.

Hii ndio hadithi ya Bernice Kariuki, Mkenya mwenye maono makubwa ambaye anahudumu kama mpishi wa binafsi wa timu ya kwanza ya klabu ya London, Arsenal.

Huku baadhi ya mashabiki sugu wa Arsenal wakiwa na ndoto ya kukutana na wachezaji wanaowaenzi siku moja, Bernice ana nafasi ya kipekee ya kuwapikia chakula.

Hadithi yake ni ya kuhusu kutia bidii, kutokata tamaa na pia ya bahati ya mtende.

Bernice alikulia mtaani Jericho katika jiji la Nairobi lakini amejijengea himaya yake kwa kusomea upishi katika Taasisi ya Westminster Kingsway jijini London.

Upendo wake kwa mapishi ulimsaidia kupata kazi katika mahoteli ya kifahari nchini Uingereza kama mpishi na amewahi kufanya kazi na mahoteli kama vile The Lanesborough, The Dorchester na The Waldorf Hilton London miongoni mwa nyingine.

Lakini kile anajivunia zaidi kwa sasa ni kuwa mpishi binafsi wa timu ya kwanza ya Arsenal, nafasi aliyopata wakati Gunners walimteua Mikel Arteta kuwa kocha wao.

Akihudumu chini ya uongozi wa Darren Taylor, Mpishi Mkuu wa Arsenal, jukumu lake Bernice ni ikiwemo kuwapikia wachezaji wa timu ya kwanza na wanachama wa ushauri na uongozi wa timu hiyo.

Udukuzi kwenye ukurasa wake wa Instagram ulitambua kwamba ni mjuzi katika kile afanyacho kutokana na picha zake alizopakia vyakula alivyopika.

Bernice, hivi majuzi alizungumza na jukwaa la Wakenya wanaoishi nchini Uingereza mjini Windsor, Berkshire mnamo Jumatatu, Novemba 29, ambapo aliwahimiza Wakenya wanaoishi ughaibuni kufuata ndoto zao bila kuwa na vijisababu.

“Ninaposhinda sote tunashinda…sote tuna changamoto. Siyo rahisi, tunahitaji kusukuma kwa sababu tuko katika nchi bora ambapo unaweza kuwa yule unataka. Usiseme kuna ubaguzi wa rangi. Hapana, hapana, hapana - unaweza kuwa yula unataka kuwa," alisema.

Akiwa katika jukwaa hilo, pia alikutana na Balozi wa Kenya nchini Uingereza, Manoah Esipisu, na balozi huyo alishindwa kuficha furaha yake.

"Nimefurahi kukutana na mpishi wa kikosi cha kwanza cha Arsenal Bernice Kariuki katika hafla ya Kenya ya Uingereza Diaspora ya sare iliyofanyika Windsor, Berkshire. Tukiwapa Wakenya moyo 'unaweza'. Hongera," mwanadiplomasia huyo alisema kwenye mtandao wake wa kijamii.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live