Wahusika wa mchezo wa Papa Shirandula walifanya hafla ya kumbukumbu katika Hoteli ya Azure, Nairobi kumkumbuka mwendazakeBeatrice Andega, mjane wa Shirandula alitoa hotuba ya huzuni akimkumbuka mume wakeAlipokuwa akizungumza, alizidiwa na hisia baada ya Jalang'o, Captain Otoyo na Njoroge kujitokeza kumsaidia binti yakeAndega alisema alikuwa anakumbwa na msongo wa mawazo kwa sababu ya kushindwa kulipa karo ya binti yake Sherry Owendi
Mnamo Julai 18, 2021, ndio inatimia mwaka mmoja baada ya kifo cha Charles Bukeko, maarufu Papa Shirandula. Shirandula aliangamizwa na COVID-19.
Wahusika wa mchezo wa Papa Shirandula walifanya hafla ya kumbukumbu katika Hoteli ya Azure, Nairobi kumkumbuka mwendazake.
Juma Anderson, ambaye aliigiza kama bosi wa Shirandula, Wilbroda mkewe wa kuigiza, Awinja mpwa wake, Kawira, Njoro na mke wake wa kuigiza Wafirethi, Otos naJalas walikuwa miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo.
Read also
Mimi Siwezi Kuolewa na Mwanamume Maskini, Asema Mwimbaji Justina Syokau
Beatrice Andega, mjane wa Shirandula alitoa hotuba ya huzuni akimkumbuka mume wake na alipokuwa akizungumza, alizidiwa na hisia baada ya Jalang'o, Captain Otoyo na Njoroge kujitokeza kumsaidia binti yake.
Andega alisema alikuwa anakumbwa na msongo wa mawazo kwa sababu ya kushindwa kulipa karo ya binti yake Sherry Owendi, ambaye anasomea katika shule ya Moi Educational Centre. Yuko katika Gredi ya Tano.
Jalang'o na wenzake waliahidi kulipa karo ya mtoto huyo hadi chuo kikuu.
Mambo yalikwenda sambamba kwene hafa hiyo na watu wengine wa familia walisema waliurahia kutambua kuwa hata kaburini, Papa Shirandula badi anapendwa.