Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Misumari iliyotumika kumsulubisha Yesu, watafiti huenda wameitambua

522257074207cf47 Misumari iliyotumika kumsulubisha Yesu, watafiti huenda wameitambua

Tue, 13 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Pasaka ni siku kuu ambayo Wakristo karibu wote hufanya kila mwaka ukumbusho wa kufufuka kwake Yesu Kristo siku ya tatu baada ya kusulubiwa kufa na kuzikwa kwake. Mwaka huu maadhimisho yalifanywa Aprili 2 hadi 3.

Lakini je, ushawahi kujiuliza misumari iliyotumika kumsulubishaYesu msalabani iko wapi?

Utafiti wa punde umeonyesha kuwa kuna misumari ya nyakati za Roma iliyohifadhiwa kwenye sanduku lililoletwa katika Chuo Kikuu cha Tel Aviv ambayo inashukiwa huenda ni misumari miwili iliyodaiwa kupotea kutoka kwenye kaburi la kuhani mkuu wa Kiyahudi Kayafa, aliyemhukumu Yesu.

Misumari hiyo miwili iliyoshika kutu ambayo baadhi wamependekeza ndiyo iliyotumika kumsulubisha Yesu msalabani inaonekana kuwa iliyotumika nyakati za kale kusulubisha, kulingana na utafiti mpya, na hali hii imezua mjadala mpevu kuhusu zilikotoka misumari hiyo.

Uchambuzi wa punde uliofanywa unasema, misumari hiyo ndiyo iliyopotea kutoka kaburi la kuhani mkuu wa Kiyahudi anayedaiwa kumkabidhi Yesu kwa Waroma kusulubiwa. Vipande vya mbao na unga kutokana na mifupa vinaonyesha kuwa inawezekana vilitumika katika kumsulubisha Yesu.

Mtaalam wa jiolojia Aryeh Shimron, mwandishi mkuu wa utafiti uliochapishwa mnamo Julai, 2020 katika jarida la Ugunduzi wa Akiolojia (Archaeological Discovery), alisema uhusiano kati ya Kayafa na ushahidi wa hivi karibuni haukuthibitisha kabisa kuwa misumari hiyo ilitumika kumsulubisha Yesu huko Yerusalemu mnamo AD 33, lakini waliimarisha madai yaliyotolewa awali.

"Kwa kweli sitaki kusema kwamba misumari hii inatokana na kusulubiwa kwa Yesu wa Nazareti," Shimron aliiambia Live Science. "Lakini ni misumari iliyotumika wakati wa kusulubiwa? Ndio, kuna uwezekano mkubwa."

Misumari hiyo ilitoka wapi?Sanduku hilo lenye mapambo ya kifahari, lililopambwa kwa nakshi za maua na kuandikwa kwa Kiaramu "Joseph mwana wa Kayafa," lilipatikana katika kaburi la karne ya kwanza huko Yerusalemu mnamo 1990. Misumari miwili ya chuma yenye kutu ilipatikana pia katika kaburi hilo, lakini baadaye ilipotea.



Israel Hershkovitz, mtaalam mashuhuri kuhusu fani ya elimu inayochunguza pande zote binadamu kuanzia wale wa kale (Anthropolojia) katika Chuo Kikuu cha Tel Aviv, alipokea misumari hiyo kwenye sanduku ambalo halikuwa na maelezo kutoka kwa mkusanyiko wa Nicu Haas, mtaalam wa anthropolojia wa Israeli aliyeaga dunia mnamo 1986.

Kulingana na Mamlaka ya Vitu vya Kale vya Israeli (IAA), Haas alivipata vitu hivyo kutoka kwenye kaburi lililochimbwa miaka ya 1970, miongo kadhaa kabla ya kaburi la Kayafa kugunduliwa, kwa mujibu wa Haaretz.

Lakini IAA haifahamu ni kaburi lipi kulipatikana misumari hiyo, na hamna stakabadhi za kuthibitisha asili zilizowahi kupatikana.

Haaretz aliripoti kwamba wasomi wengine, ingawa hakutaja majina, wameita utafiti wa hivi karibuni kuwa wa kukisia tu.



Wafanyakazi waliokuwa wakipanua barabara waligundua kaburi la "Kayafa" la karne ya kwanza mnamo 1990 katika kitongoji cha kusini mashariki mwa Yerusalemu. Kaburi hilo lilikuwa na masanduku 12 - - moja lililowekwa alama ya jina "Qayafa" na nyingine, iliyopambwa kwa mapambo ya maua, yaliyoandikwa kwa Kiaramu "Yehosef Bar Qayafa," au "Joseph mwana wa Kayafa" kwa Kiingereza. Wanaakiolojia wengi sasa wanakubali kwamba kaburi hilo lilitumika kumzika kuhani mkuu wa karne ya kwanza Kayafa na familia yake, utafiti huo ulisema.

Kayafa, ambaye anatajwa mara kadhaa katika Agano Jipya la Kikristo na historia ya Wayahudi iliyoandikwa mwishoni mwa karne ya kwanza na Flavius ​​Josephus, alisimamia kesi ya 'kijinga' ya Yesu kwa kukufuru, baada ya hapo Yesu alikabidhiwa kwa gavana wa Kirumi Pontio Pilato ili kunyongwa, kulingana na Injili ya Mathayo.

Utekelezaji huo uliripotiwa kufanywa Ijumaa Aprili 3, 33, wakati Yesu alipopigiliwa msalabani - njia iliyokuwa ya kawaida ya adhabu ya kifo kwa Warumi.

Mwandishi ni Ali Hassan Kauleni, Kaunti ya Nairobi

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke