Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Misri yatoa matamshi ya chuki dhidi ya Israel licha ya mkataba wa amani - Jerusalem Post

Misri Yatoa Matamshi Ya Chuki Dhidi Ya Israel Licha Ya Mkataba Wa Amani   Jerusalem Post Misri yatoa matamshi ya chuki dhidi ya Israel licha ya mkataba wa amani - Jerusalem Post

Wed, 5 Jun 2024 Chanzo: Bbc

Gazeti la Israel la The Jerusalem Post lilichapisha makala inayokosoa msimamo wa Misri kuhusu vita vya sasa vya Gaza, na kusema kuwa Cairo inachapisha "ujumbe wa chuki dhidi ya Israel" licha ya mkataba wa amani kati ya nchi hizo mbili.

Makala iliyoandikwa na Ruth Wasserman Land, naibu balozi wa zamani nchini Misri, ilisema kuwa Misri inatekeleza sera ya nchi mbili, kwa kushirikiana na Israel na wakati huo huo, kueneza ujumbe wenye uadui nayo.

Ruth alisema kuwa Misri imetia saini mkataba wa amani na Israel na inajitahidi kuanzisha njia za kibiashara na kushirikiana na Marekani, lakini kwa upande mwingine inatoa ujumbe ambao unachukia Israel kwa raia wa Misri.

Alieleza kuwa kwa mtazamo wa Misri, "kuanzishwa kwa taifa la Palestina ilikuwa nguzo ya msingi ya makubaliano ya amani, na kushindwa kufikiwa kwa hili kuliruhusu utawala wa Misri unaoongozwa na Mubarak kujizuia kuimarisha ushirikiano wa pande mbili na Israel katika nyanja za biashara, utamaduni, utalii na mengineyo."

Mwandishi aliongeza kuwa Misri "inakubali maneno ya kupinga Israel," na kwamba uongozi wa Misri uliruhusu, na wakati mwingine kuhimiza, kupitishwa kwa maneno ya chuki dhidi ya Israel, "kama njia ya kuvuruga maoni ya umma kutoka kwa matatizo ya ndani."

Chanzo: Bbc