Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Misri na Marekani zakubali kuruhusu msaada kuingia Gaza

Misri Na Marekani Zakubali Kuruhusu Msaada Kuingia Gaza Misri na Marekani zakubali kuruhusu msaada kuingia Gaza

Thu, 19 Oct 2023 Chanzo: Bbc

Rais Joe Biden wa Marekani na Abdel Fattah al-Sisi wa Misri wamekubali kufungua kivuko cha Rafah ili kuruhusu hadi lori 20 za misaada kuingia Gaza.

"Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi na Rais wa Marekani Joe Biden wamekubaliana juu ya utoaji endelevu wa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza kupitia kituo cha Rafah," alisema msemaji wa rais Ahmed Fahmy katika taarifa.

Mazungumzo kati ya viongozi hao wawili yalisema msaada huo utaratibiwa na mamlaka husika katika nchi hizo mbili zenye makundi ya kimataifa ya kibinadamu, chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa.

Usafirishaji huo labda hautapita Ijumaa, Biden alisema, akitoa mfano wa ukarabati wa barabara.

"Watatengeneza barabara, wanapaswa kujaza mashimo ili kupata lori hizi ziweze kupita. Na hilo litafanyika - wanatarajia itachukua takriban saa nane [Alhamisi]. Kwa hivyo kunaweza kuwa hakuna kitu kinachoendelea hadi...pengine hadi Ijumaa,” aliwaambia wanahabari siku ya Jumatano.

Aliongeza kuwa lori hizo 20 ziliwakilisha "hatua ya kwanza" lakini akasema lori "150 hivi" kwa jumla zilikuwa zikisubiri. Ikiwa wale waliruhusiwa kuvuka au la itategemea "jinsi itakavyokuwa".

Mashirika ya kimataifa ya misaada yanasema hitaji la msaada ni la dharura.

Chanzo: Bbc