Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mimi ndio Magufuli wa Kenya, Raila Odinga asema kuhusu safari ya Ikulu

Fbd833f634c41622 Mimi ndio Magufuli wa Kenya, Raila Odinga asema kuhusu safari ya Ikulu

Sun, 13 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Raila alisema serikali yake itapambana na ufisadi vikali ili kufungu mapengo yanayotumiwa kula mfuko wa mlipa ushuru

- Aliahidi kuleta mfumo kama ulioendeshwa na aliyekuwa rais wa Tanzani John Pombe Magufuli

- Alitaka waungane na Kalonzo ili kufufua muungano wao wa 2013 na 2017

Kinara wa ODM Raila Odinga amesema ataleta mageuzi makubwa serikalini akiingia Ikulu kumrithi Rais Uhuru Kenyatta.

Raila alisema Kenya ni nchi tajiri lakini kuna mafisi serikalini ambao wanapora mifuko ya umma na kujitajirisha.

Aliahidi kuleta mageuzi makali kama yaliyoletwa nchini Tanzania na aliyekuwa rais John Pombe Magufuli.

Akiongea wakati wa mazishi ya mwanasiasa Kalembe Ndile Makueni, Raila alisema watakabiliana na ufisadi ili wananchi wafaidike.



Alisema fedha zinazotolewa na wananchi kama ushuru huliwa na wachache uongozini.

"Inawezekana tutoe mamilioni ya watu kutoka ufukara mpaka wawe matajiri. Inawezekana tukibadili mambo

"Tuko na bajeti ya trilioni tatu na bilioni sita lakini mingi itaenda kwa mifuko ya watu ambao wanaiba. Wananunua manyumba Nairobi na wananchi wanataabika," alisema Baba.



Alisifu uongozi wa Magufuli nchini Tanzania na kuahidi kutekeleza mfumo wake humu nchini ili kukabili wakora serikalini.

"Kitu tutafanya ni kuziba mianya na maendeleo yataanza kufanyika . . . Magufuli alifanya hayo hapa Tanzania. Na mumeona iliyofanyika ndani ya miaka mitano," alisema Baba.

Ilikuwa mara ya kwanza kwa Raila, tangu aingie kwenye handisheki, kuzungumzia kuhusu uwezekano wake kuwania urais 2022.

Raila alisema yuko tayari kufanya kazi na Kalonzo ili kuingia Ikulu 2022 akiashiria kuna mipango inayoendelea faraghani.

"Mimi na Kalonzo hatuwezi kukosana. Tutakubaliana tu . . . tutasimama pamoja ili tuweze kutoa hawa wezi ambao wanadanganya Wakenya. Mimi bnataka Wakenya wasimame imara," alisema Baba.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke