Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Miguna atabiri Ruto kumchakaza Raila kwenye Uchaguzi Mkuu 2022

7016b7a1b8ae495c Miguna atabiri Ruto kumchakaza Raila kwenye Uchaguzi Mkuu 2022

Tue, 7 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wakili aliyefurushwa nchini Miguna Miguna amedai kuwa Naibu Rais William Ruto atamshinda Raila Odinga iwapo wawili hao watamenyana kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2022.

William Ruto ametangaza azma yake ya kumrithi Rais Uhuru Kenyatta na amekuwa akijipigia debe kupitia vuguvugu la hasla linalolenga mfumo wa kiuchumi wa bottom-up.

Mnamo Jumapili, Agosti 22, Raila Odinga pia alitangaza rasmi kuwa atajitosa kwenye kivumbi hichoWakili mwenye utata Miguna Miguna alisema Uhuru, Raila na Mpango wa Maridhiano (BBI) walimupa Ruto umaarufu

Miguna alisema Ruto atashinda uchaguzi hizo mapema asubuhi.

"Sijawahi fanya makosa katika mambo ya siasa. Ndio maana Moi alinitimua nchini 1987 na Raila Odinga aliniomba nimshauri mwaka 2006 na 2017. ndio maana Uhuru Kenyatta ananiogopa sana. Sikia hii William Ruto atamshinda Raila kufikia saa nne asubuhi," alidai.

Wakili huyo mwenye utata alisema Uhuru, Raila na Mpango wa Maridhiano (BBI) walimupa Ruto umaarufu

"Usimlaumu William Ruto. Wanasiasa wote hutafuta kuungwa mkono. Laumu Uhuru Kenyatta, Raila Odinga na BBI kwa Ruto kuwa maarufu. Bahati mbaya kwao, wamechelewa.Huo ndio ukweli. Wale wanataka kunitusi mnaweza nitusi. Sishtuki," aliongezea.



Wakili huyo anayeishi nchini Canada alisema mpango wa Uhuru na Raila kushinikiza kupitishwa kwa BBI licha ya mahakama kuharamisha haungelikuwa sawa.

Alihoji kuwa mswada wa BBI haukuwa na umaarifu a haungepita kicha ya jhudi za waiwli hao.

Miguna alimkashifu Raila kwa kumsaliti baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2017 alipomuapisha kama rais wa watu bustani la Uhuru Park, Nairobi, Januari 30, 2018.

Kampeni za RutoRuto ametangaza azma yake ya kumrithi Rais Uhuru Kenyatta na amekuwa akijipigia debe kupitia vuguvugu la hasla linalolenga mfumo wa kiuchumi wa bottom-up.

Akizungumza Jumapili, Septemba 5, eneo la Kieni, kaunti ya Nyeri, Ruto alisema wakati umewadia wa kubadilisha maisha ya Wakenya.

Alisema ataendelea na mazungumzo ya kushughulikia matakwa ya wananchi bila kujali vyeo.

Mnamo Jumapili, Agosti 22, Raila Odinga pia alitangaza rasmi kuwa atajitosa kwenye kivumbi hicho.

Tangazo la Rail, lilijiri siku moja tu baada ya Mahakama kutupa rufaa kuhusu mswada wa BBI.

"Kwa miezi nimekuwa nikiskia watu wakipiga kelele kuhusu wheelbarrow. Wamekuwa na wakati wakutosha kufanya hivyo, sasa wakati umefika tukutane nao kwenye uwanja," alisema Raila.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke