Mechi kati ya Liverpool na Man City ilishuhudia timu zote mbili zikigawana mkate na kutoka droo ya 2-2 City ilitoka nyuma mara mbili katika awamu ya pili na kuchomoa pointi ugeniniMane na Salah ndio walifungia Liverpool mabao, huku Foden na De Bruyne wakifungia City Matokeo hao yalishuhudia Chelsea ikipaa kileleni mwa jedwali wikendi na alama 16, pointi moja mbele ya Reds Mechi ya Ligi Kuu Uingereza ya Liverpool dhidi ya Man City, ilitamatika sare ya 2-2 huku miamba hao wawili wakigawana pointi ugani Anfield.
Mechi hiyo ya Jumapili, Oktoba 3, ilishuhudia City wakitoka nyuma mara mbili na kuchomoa pointi kutoka kwa Merseysiders.
Huku timu zote mbili zikifurahia pointi hiyo, City watajutia kupoteza nafasi za wazi wakiongoza mchezo huo katika awamu ya kwanza.
Nafasi ya kupaa kileleni mwa jedwali ilikuwa inayumba wakati timu hizo zilikuwa zikivaana huku mabingwa watetezi wakihitaji ushindi wa 2-0 kupiku Chelsea uongozini.
Wakati huo huo Liverpool walikuwa wanatafuta ushindi wa kurejesha nafasi yao ya kuongoza jedwali.
Kevin de Bruyne alikaribia kufunga dakika taatu baadaye baada ya kumegewa pasi tamu lakini alishindwa kulenga shaba.
Awamu ya pili ndio ilikuwa kilele cha mchezo huo timu zote zikifunga mara mbili huku Sadio Mane akifungua ukurasa wa mabao kunako dakika ya 59.
Hata hivyo, Foden alisawazishia timu yake dakika 10 baadaye na kufanya mambo kuwa 1-1.
Kocha wa Watforf afutwa kaziAwali, TUKO.co.ke iliripotia kuwa kocha wa Watford, Xisco Munoz amepigwa kalamu na klabu hiyo ya Vicarage Road.
Hornets wamepoteza mechi sita walizoshiriki msimu huu na kushinda mbili pekee na kushikilia nafasi ya 14.
Munoz aliajiriwa na klabu hiyo Disemba 2020, na aliwasaidia kupandishwa ngazi kuingia Ligo Kuu Uingereza.