Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mgonjwa aliyetoweka katika Hospitali ya Mbagathi apatikana amefariki

300d8ba9f4e0a921 Mgonjwa aliyetoweka katika Hospitali ya Mbagathi apatikana amefariki

Mon, 26 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Jane Kari alilazwa katika Hospitali ya Mama Lucy mnamo Julai 12 Mume wake, Naftaly alipokea simu usiku wa manane akifahamishwa kuwa mke wake amehamishwa hadi Hospitali ya MbagathiKisha baadaye aliambiwa na madaktari wa Mbagathi kuwa atamuona Jane baada ya siku sabaSiku saba baadaye famila hiyo ilimpata jamaa wao katika makafani ya Hospitali ya Mbagathi

Familia moja mtaani Kayole, Nairobi inaomboleza kifo cha jamaa wao ambaye alifariki katika hali tatanishi siku moja baada ya kulazwa katika Hospitali ya Mama Lucy.

Jane Kari alilazwa katika Hospitali ya Mama Lucy mnamo Julai 12, na mume wake, Naftaly alipokea simu usiku wa manane akifahamishwa kuwa mke wake amehamishwa hadi Hospitali ya Mbagathi kwa sababu ya matatizo ya COVID-19.

Akizungumza na Citizen TV, mjane huyo alisema alifahamishwa na madaktari wakitumia simu ya Jane kuwa mke wake alihamishwa kwa sababu ya kukosekana kwa oksijeni.



Read also

Isiolo: Afisa Aliyerusha Bomu Akimlenga "EX" Wake Akosa Shabaha na Kulipua Nyeti za Mwanajeshi

Kisha baadaye aliambiwa na madaktari wa Mbagathi kuwa atamuona Jane baada ya siku saba kwa sababu alikuwa amewekwa karantini.

"Nilisubiri. Siku saba ziliisha Jumanne lakini hawakunipigia. Nilisubiri simu yao kwa siku mbili zaidi lakini sikupata. Mnamo Alhamisi nilienda hospitalini na kumpata daktari mwingine ambaye aliniambia mke wangu hayupo kwenye wodi.Nilimtafuta wodi mzima lakini sikumuona," alisema Naftaly.

Ni hadi mnamo Jumamosi, Julai 24, ndipo familia hiyo ilitambua kuwa mwili wa Jane ulikuwa makafani.

Huku msako wa mama huyo mwenye umri wa miaka 57, uliishia kuwa mauti, familia yake imewachwa na maswali tumbi nzima ikitaka kujua namna mwili wa Jane ulipatikana makafani licha ya kufahamishwa kwamba alikuwa amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Kikosi cha mawasiliano cha Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta kimehakikishia familia hiyo kuwa kitabainisha kilichotokea.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.



Read also

Jamaa Akamatwa Lamu Akiwa Amevalia Mavazi ya Kike, Aambia Polisi Ana Mradi wa Kubuni mabawa
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke