Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mfungwa Aliyepatikana na Coronavirus Aaga Dunia Akiwa Katika Seli

B33d6bf3b0734d52 Mfungwa Aliyepatikana na Coronavirus Aaga Dunia Akiwa Katika Seli

Tue, 6 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mfungwa wa kiume mwenye umri wa miaka 32 ambaye hivi alipimwa na kupatikana na COVID-19 aliaga dunia kwenye seli ya polisi huko Kuria Magharibi, Kaunti ya Migori, Jumatatu.

Ripoti ya polisi ilionesha kuwa mfungwa aliyetambuliwa kwa jina la Samwel Marwa ambaye alihukumiwa Aprili 1, 2021, alipimwa na kuthibitishwa kuugua ugonjwa huo amekuwa chini ya uangalizi wa maafisa wa afya.

Kamanda wa Polisi kaunti ndogo ya Kuria Magharibi Cleti Kimaiyo alisema mtuhumiwa huyo hangepelekwa katika Gereza la Migori GK kwa sababu ya hali yake ya COVID-19 kwa hivyo alitengwa katika seli.

Kulingana na ripoti ya Citizen Digital, Kimaiyo alisema mfungwa huyo alikuwa akiendelea kupata nafuu hadi Jumapili saa nane adhuhuri wakati alipozimia na kuanza kutokwa ma povu mdomoni.

Alidokeza kuwa maafisa wa afya waliitwa mara moja wakamshughulikia mfungwa huyo akiwa kizuizini hadi pale ambapo hali yake ya afya ilipoimarika.

Hata hivyo ilipofika Jumatatu majira ya saa moja asubuhi, maafisa waliokuwa wakishika doria walimkuta akiwa amefariki dunia.

Kamanda huyo alisema wangali wanasubiri ripoti zaidi ya matibabu ili kubaini kiini haswa cha kifo chake.

Familia ya marehemu imearifiwa kuhusu kifo cha mpendwa wao ambapo tayari wanafanya mipango ya kuupeleka mwili wake katika makafani ya hospitali ya Migori Level Four.

Aidha aliongeza kuwa watashirikiana na maafisa kutoka idara ya afya ili kulupiza dawa katika seli hiyo.

Marehemu alikuwa amefungwa kwa miezi sita au kulipa faini ya KSh 10,000 baada ya kupatikana akiuza pombe haramu eneo la Kuria Magharibi.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke