Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mfu azikwa usiku baada ya familia kufumaniwa na polisi ikiendesha mkesha

0fgjhs1i5ak7od42s Mfu azikwa usiku baada ya familia kufumaniwa na polisi ikiendesha mkesha

Fri, 23 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Familia moja kaunti ya Homa Bay ilipatikana ikiandaa mkesha wa usiku wa mpendwa wao Jumatano, Julai 21Polisi waliishurutisha familia hiyo kumzika mwanamke huyo kwa kukiuka maagizo ya kudhibiti maambukizi ya COVID-19Chifu wa eneo hilo alishikilia kwamba kulingana na masharti ya COVID-19, mfu anapaswa kuzikwa siku ambayo mwili wake unaondolewa kwenye makafaniFamilia katika kijiji cha Kakur eneo la Ndhiwa, kaunti ya Homa Bay mnamo Jumatano, Julai 21 walilaazimika kumzika mpendwa wao usiku wa manane baada ya kunaswa wakiandaa mkesha.

Marehemu Mary Atieno mwenye umri wa miaka 25 aliyefariki siku chache zilizopita alizikwa chini ya uangalizi wa maafisa wa polisi kutoka kituo cha Pala na chifu ambaye alisema familia hio ilikiuka itifaki za COVID-19.

Polisi walikuwa wamepokea habari kutoka kwa mzee wa kijiji kwamba familia ilikuwa inaandaa kabla ya mazishi ya marehemu ambayo yalipangwa Alhamisi, Julai 22.

Mwili wa Mary ulifika nyumbani kwake usiku wa Jumatano baada ya kusafirishwa kutoka makafani katika eneo la Kamagambo huko Rongo.



Read also

Isiolo: Afisa Aliyerusha Bomu Akimlenga "EX" Wake Akosa Shabaha na Kulipua Nyeti za Mwanajeshi

TUKO.co.ke ilizungumza na chifu wa eneo la Boya Milton Kawino ambaye alisema yeye pamoja na polisi walivamia boma hilo saa tisa usiku na kukuta familia ikiendelea na kinyume na kanuni za COVID-19.

Chifu huyo alishikilia kwamba mfu anapaswa kuzikwa siku ambayo mwili wake unaondolewa kwenye makafani.

Maafisa wa polisi waliwashurutisha jamaa kuchimba kaburi na kumzika mpendwa wao.

Chifu huyo aliwaonya vikali wenyeji wa eneo hilo kuzingatia maagizo yaliyowekwa na serikali ili kudhibiti maambukizi ya COVID-19.

Awali iliripotiwa kuwa, Rais Uhuru Kenyatta aliongeza muda wa kafyu katika maeneo 13 yaliyoko kwenye hatari ya msambao wa maradhi hayo hatari.

Kaunti hizo 13 zilijumuisha Busia, Vihiga, Kisii, Nyamira, Kakamega, Kericho, Bomet, Bungoma, Trans-Nzoia, Kisumu, Siaya, Homa Bay na Migori.

Taarifa yake Zabibah Adhiambo, mwandishi wa TUKO.co.ke

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.



Read also

Askari Jela Akamatwa kufuatia Tuhuma za Visa vya Utekaji Nyara
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke