Wed, 13 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mfalme wa Morocco Mohammed VII ameonesha mshikamano kwa taifa lake lililo kwenye majonzi kwa kuchangia damu na kuwatembelea baadhi ya majeruhi katika hospitali moja mjini Marrakesh
Aidha, raia wa Morocco wamekuwa wakijitoa huko Marrakesh na katika miji mingine kwa kuwachangia damu majeruhi.
Aidha, baadhi ya raia wa Morocco wameilaumu serikali kwa kucheleweshewa huduma za uokoaji.
Zaidi ya watu 2,900 wamefariki kutokana na tetemeko hilo huku wengine zaidi ya 5,500 wakiachwa na majeraha mbalimbali.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live