Waumini wa kanisa moja hapa walibaki vinywa wazi pasta wao alipomkemea mkewe mbele yao.
Pasta huyo alimsimamisha mkewe mbele ya kanisa na kumtaka aeleze alivyotumia pesa za hazina ya kina mama.
Mhubiri huyo alimchemkia mkewe akimtaja kama mtu asiyeaminika. Alidai mkewe alikuwa amehusika na kupotea kwa pesa za kina mama na kuapa kumchukulia hatua kali.
“Badala ya kusaidia mipango ya kina mama kutimia, unakuwa wa kwanza kutumia hela hizo kwa mipango yako binafsi. Rudisha pesa za wenyewe ama nichukue hatua,” aliwaka pasta.
Mama huyo alitoka nje ya kanisa akiwa ameaibika mbele ya waumini.
Kulikuwa na hisia mseto kanisani humo huku baadhi ya waumini wakimkosoa kwa kumdhalilisha mke wake mbele yao na wengine wakifurahia uadilifu wake wa hali ya juu ambao ulimfanya akemee mke mporaji.