Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mchungaji afariki akifukuza mapepo

Daniel Naheirwe Mchungaji afariki akifukuza mapepo

Thu, 26 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Polisi wameanzisha uchunguzi kuhusu kisa ambapo pasta maarufu wa kanisa la Pentekoste alifariki katika mazingira yasiyoeleweka.

Kulingana na ripoti ya polisi, mhubiri huyo mwenye makao yake makuu mjini Kampala alipoteza maisha yake alipokuwa akijaribu kuchoma moto tunguri ambazo zilizodaiwa kuwa na mapepo.

Gazeti la The Monitor liliripoti kuwa Mchungaji Daniel Naheirwe alifariki Jumanne, Oktoba 24, nyumbani kwa mmoja wa wafuasi wake, Jessica Kyohairwe, ambako aliripotiwa kuwatimua mapepo wachafu.

"Kesi ya kifo cha ghafla imeripotiwa. Kikosi cha wapelelezi kilitembelea eneo la tukio na kufanya uchunguzi. Askari wa upelelezi walifanya upekuzi, na Itel, simu ya mkononi ilichukuliwa kutoka kwake.

"Taarifa husika kutoka kwa mashahidi husika zilirekodiwa, na maiti ilifikishwa Nakasongola HCIV kwa upasuaji huku askari wakiwatafuta jamaa zake," taarifa ya polisi ilisoma.

Kulingana na mmiliki wa nyumba hiyo, mtumishi huyo wa Mungu alisafiri kutoka Kampala hadi nyumbani kwake makusudi kuharibu vifaa vya uchawi na pia kumwombea muumini wake.

Aliwaambia polisi kwamba Daniel alianguka na kufa papo hapo alipokuwa akichoma vitu vinavyoshukiwa kuwa vya uchawi.

“Alifanya maombi na kufanya miujiza yake, kisha akaitoa ile mizimu. Baadaye alichukua moto na kuteketeza mboga na vitu walimokuwa wamewekwa wale wanaodaiwa kuwa ni pepo wachafu. Kwa bahati mbaya wakati wa kuungua alianguka na kufariki dunia papo hapo,” Naheirwe aliwaambia polisi.

Mwili wa pasta huyo ambaye ni maarufu miongoni mwa wafuasi wake kwa kuchoma vitu vinavyoshukiwa kutumika kwa uchawi, ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti, ukisubiri kufanyiwa upasuaji.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live