Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mchungaji adai watu ambao hawajaokoka hawapaswi kutoa sadaka

Tony Kiamah.jpeg Mchungaji adai watu ambao hawajaokoka hawapaswi kutoa sadaka

Mon, 10 Oct 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mchungaji mmoja Mkenya amewaonya watenda dhambi dhidi ya kutoa sadaka zao kanisani.

Mchungaji Tony Kiamah alisema kuwa pesa za watu ambao hawajaokoka hazina manufaa kwa kanisa kwani hazina thamani yoyote.

Katika video iliyosambaa sana baada ya kupakiwa kwenye Facebook, Kiamah alisema watu ambao hawajaokoka wanatakiwa kutoa tu nyoyo zao kwa wokovu.

"Kama haujaokoka tafadhali kaa an hela zako kwa upole na kwa kukubembeleza. Hazina manufaa yeyote kabisa mbele za Mungu. Hela za mtenda dhambi hazina kazi. Mungu anapendezwa zaidi na roho yako, sio pesa zako," alisema Kiama.

Mahubiri yake yalizua gumzo kwenye mitandao ya kijamii huku baadhi ya wanamtandao wakimsifu nao wengine wakisema kuwa amewasahau wahubiri waroho.

Carolyn Mbotho aliandika: "Ina nguvu sana. Watu wanahitaji kusikia hili. Amina kwa mahubiri."

Triza Favour Ngugi aliandika: "Pesa inapendwa sana na mioyo ya wanadamu. Na ninaamini watu wengine wanatoa kwa sababu wana moyo wa Mungu tu kwamba wanataka maisha mawili ambapo unaweza kufanya dhambi na bado ukawa kanisani."

Jonathan Kibet aliandika hivi: “Mchungaji Endelea kuhubiri ukweli kwa wote kwa sababu kila kitu ni cha Mungu na Mungu anahitaji tu nafsi zetu zinazompenda Amina.

James Muthike aliandika: "Huwezi kubadilisha utii wako badala ya kutoa au sadaka au dhabihu."

Vinny Skinton aliandika: "Tunakosa wahubiri wa aina hii, natamani ningekua karibu ningehudhuria ibada hii kila Jumapili."

Chanzo: www.tanzaniaweb.live