Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbunge wa Kenya alaumiwa kwa kuvaa skafu ya Palestina

Mbunge Wa Kenya Alaumiwa Kwa Kuvaa Skafu Ya Palestina Mbunge wa Kenya alaumiwa kwa kuvaa skafu ya Palestina

Thu, 26 Oct 2023 Chanzo: Bbc

Mbunge wa Kenya aliamriwa kuvua skafu ya kitamaduni ya Wapalestina aliyokuwa amevaa wakati wa vikao vya bunge siku ya Jumatano.

Farah Maalim alisema alikuwa amevaa skafu hiyo kwa mshikamano na Wapalestina mjini Gaza, huku kukiwa na mapigano kati ya Israel na Hamas.

Alisema Palestina "inahitaji kuungwa mkono na kila mtu nchini Kenya".

Lakini spika wa Bunge la taifa aliamuamuru mbunge huyo kuvua skafu akisema vazi hilo linakiuka kanuni za bunge.

Wabunge wenzake pia walimlaumu mbunge huyo kwa "kutoheshimu" kanuni za Bunge.

Haya yanajiri siku chache baada ya polisi nchini Kenya kuwazuilia watu watatu kwa muda mfupi kwa kushiriki katika mkutano watu wanaoiunga mkono Palestina katika mji mkuu, Nairobi.

Rais William Ruto ameeleza kuunga mkono kikamilifu wa serikali yake kwa Israel katika mzozo unaoendelea.

Chanzo: Bbc