Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbunge mbaroni kwa kumshambulia mpiga kura

Mika Mbunge mbaroni kwa kumshambulia mpiga kura

Wed, 10 Aug 2022 Chanzo: dar24.com

Mbunge wa Nakuru Mjini Mashariki, David Gikaria ametiwa mbaroni kwa madai ya kuwashambulia wapiga kura.

Kamanda wa polisi kaunti ya Nakuru, Peter Mwanzo amethibitisha kukamatwa kwa mbunge huyo na kusema anatuhumiwa kumvamia na kumjeruhi mpiga kura katika kituo cha kupigia kura katika eneo la jimboni kwake.

Gikaria alikamatwa katika kituo cha kupigia kura cha Shule ya Msingi ya Naka kufuatia ghasia aliyoifanya akiwa katika eneo hilo.

“Tulimkamata baada ya kumvamia na kumjeruhi mpiga kura na pia amezua tafrani na fujo katika kituo cha kupigia kura na hatutakubali hilo,” amesema Mwanzo.

Mpiga kura huyo aliyeshambuliwa alilazwa hospitalini akiwa na majeraha kichwani.

Gikaria anazuiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Nakuru.

Chanzo: dar24.com