Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbunge atimuliwa katika hafla ya mazishi

658f66e85e55442b Mbunge atimuliwa katika hafla ya mazishi

Sun, 1 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mbunge wa Bomachoge Chache Alpha Miruka alilazimika kukimbilia usalama wake baada ya wenyeji wa eneo bunge lake kumtimua katika mazishi Ijumaa, Julai 30Wakazi hao walikuwa wakilalamika kuhusiana na kujikokota kwa maendeleao katika eneo lao na wakataka kupewa majibu kuhusiana na suala hiloMakundi mawili ya waombolezaji walikabiliana wakati mwanasiasa huyo alipowasili huku wakitupiana vitiMbunge wa Bomachoge Chache Alpha Miruka alilazimika kukimbilia usalama wake baada ya wenyeji wa eneo bunge lake kumtimua katika mazishini Ijumaa, Julai 30.

Kwenye video iliyokuwa ikitamba mitandaoni wakazi hao walikuwa wakilalamika kuhusiana na kujikokota kwa maendeleao katika eneo lao na wakataka kupewa majibu kuhusiana na suala hilo.

Makundi mawili ya waombolezaji walikabiliana katika mazishi hayo wakati mwanasiasa huyo alipowasili huku wakitupiana viti.

Baadhi yao hata walionekana wakiwaza makonde walioukwa wakmitetea mbunge huyo.

Mbunge huyo alikabiliwa na shutuma kutoka kwa vijana waliokuwa na hamaki waliomtaka kuondoka katika hafla ya mkazi aliyepoteza maisha yake katika ajali ya barabarani.

Read also

Didmus Barasa Akanusha Alimlima Kofi Steve: "Nilikuwa Namuashiria Afunge Zipu Yake"

"Hatujafurahishwa hata kidogo. Tunataka maendeleo, kujengewa barabara na miondombinu msingi. Mwacehni ende! Hatumtaki hapa!" baadhi ya vijana walisikika wakisema huku walinzi wa mwanasiasa huyo wakiharakisha kimwingiza ndani ya gari.

Shughuli katika hafla hiyo zilisimamishwa kwa muda baada ya baadhi kuvunja viti na hata kubomoa mahema.

"Mbunge wetu anapaswa kuishurutisha serikali kutujengea barabara sisi tumchoka kusubiri," kijana mmoja alilalamika.

Hata hivyo maswali yaliibuka ya ni wapi maafisa wa kulinda usalama walikokuwa wakati wa purukushani hiyo.

Walinzi wa mbunge huyo walidai kwamba sarakasi hizo zilipangwa na maadui wake ambao wanawachochea wenyeji kumtimua Uchaguzi Mkuu wa 2022 unapokaribia.

"Wamekuwa wakimpiga vita kisiasa. Walizua sarakasi na nikaona ni busara niondoke. Hii sio mara ya kwanza nashambuliwa," mbunge Miruka alisema huku akijaribu kuwatuliza vijana.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke