Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbunge Wambugu Ngunjiri asema Jubilee imeimarika bila DP Ruto

A2e98f62232e1e86 Mbunge Wambugu Ngunjiri asema Jubilee imeimarika bila DP Ruto

Thu, 17 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Jumanne, Juni 15, Naibu Rais William Ruto alichapisha ujumbe Twitter akimshtumu Rais Uhuru Kenyatta baada ya kuashiria atamuunga mkono mgombea urais wa NASAMwanasiasa huyo mwenye utata, alisema kwamba kwa msaada wa Mungu hatakata tamaa katika azimio lake la kuingia IkuluMbunge wa Nyeri Town Ngunjiri Wambugu alisema chama tawala cha Jubilee kilikuwa bora bila DP Mbunge wa Nyeri Mjini Ngunjiri Wambugu amemtaka Naibu Rais William Ruto kujiondoa katika chama tawala cha Jubilee baada ya kuwaka moto mnamo Jumanne, Juni 15.

Kwenye jumbe zake Facebook, mwanasiasa huyo wa Jubilee alisema kwamba chama tawala kwa sasa kimeimarika hata zaidi baada ya Naibu Rais kuondoka kimyakimya.

"Ruto anapaswa kuambiwa Jubilee kama vile Oranga Democratic Movmenet ( ODM)- haitaangamia kwa sababu eti ameondoka. Hebu aambiwe kwamba kuondoka kwake hakujaathiri Jubilee kwa njia yoyote. Aliondoka ODM lakini chama hicho kikasalia kuwa imara hata zaidi. Mwanzo vyama vyote viliimarika hata zaidi baada yake kuondoka," Wambugu alisema.

Mbunge huyo ambaye ni mtetezi wa utawala wa Jubilee, alimtaka Ruto ajiuzulu kutoka kwa chama hicho na kujenga chama cha United Democratic Alliance ambacho amekikumbatia waziwazi.

"Anaendelea kuwaambia watu wafuate katiba. Je! Sio yeye afanye hivyo na ajiuzulu kutoka Jubilee na aingie rasmi UDA? Hata Mungu hapendi watu ambao hawana msimamo!" mbunge huyo alisisitiza.

Matamshi ya Wambugu yanajiri baada ya Ruto kukejeli mpango wa Rais Uhuru Kenyatta wa kumuunga mkono mgombea urais wa National Super Alliance (NASA) katika Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Huku akionekana kutoa maoni yake kuhusiana na taarifa iliyochapishwa na mojawapo ya magazeti humu nchini kwamba kiongozi wa taifa atamuunga mkono mmoja wa vigogo wa NASA, Ruto alishangaa ni wapi Wakenya milioni 8 waliowaunga mkono wataelekea.

Mwanasiasa huyo mwenye utata, alisema kwamba kwa msaada wa Mungu hatakata tamaa katika azimio lake la kuingia Ikulu.

"Eucho! Ngai fafa mwathani !! Kwa hivyo, ni nini kinachowatendekea Thurakus, kikosi cha kumìrà kùmèrà, watu wetu milioni nane? Hamna, hamna kijana, hamna mwanamke, hamna mtu yeyote kati ya milioni nane walioamka mapema kuwapiga UK /WsR atakumbukwa hapa? Sawa tu! Tutapanga mikakati na msaada wa Mungu."

Wambungu akijibu matamshi ya Ruto alisema kwamba hapaswi kulalamika kwa sababu amekuwa akiwasimamisha wagombea wake uwanjani kinyume na Jubilee wakati bado anaongoza katika serikali ya chama hicho tawala.

"Kwa hivyo huyu jamaa amekuwa akisimamisha wagombea dhidi ya chama cha rais ili kumdhoofisha Uhuru, lakini sasa anashangaa wakati jarida linasema Uhuru anaweza kumuunga mkono mgombea mwingine badala yake?" Wambugu alidokeza.

Mnamo Machi 2021, Ruto alifichua kwamba ana mpango mbadala iwapo atafukuzwa Jubilee kama naibu kiongozi wa chama hicho.

Mwanasiasa huyo alifichua kwmaba atatumia UDA kama gari lake 2022 la kumpelea Ikulu wakati wa Uchaguzi Mkuu.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke