Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbunge Kenya kusota rumande kwa siku saba

92563 Pic+kenya Mbunge Kenya kusota rumande kwa siku saba

Wed, 22 Jan 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Nairobi, Kenya. Mahakama Kuu nchini Kenya, imeamuru mbunge wa upinzani nchini Kenya, Paul Ongili maarufu Babu Owino  kuendelea kukaa rumade kwa siku saba zaidi.

Babu Owino ameshtakiwa kwa kosa la jaribio la kuua kwa kukusudia baada ya kumpiga kwa risasi DJ katika ukumbi wa muziki.

Jaji Francis Andayi leo Jumanne Januari 21 aliagiza mbunge huyo aendelee kukaa kizuizini kwa siku saba zaidi hadi ombi lake la kutaka kuachiwa kwa dhamana litakaposikilizwa.

Jaji Andayi alisema endapo mbunge huyo atapewa dhamana kwa sasa anaweza kuharibu uchunguzi kwa kuwarubuni mashahidi wa kesi hiyo.

Ijumaa iliyopita, mbunge Owino alikamatwa na polisi kwa tuhuma za kumpiga risasi DJ mmoja baada ya kutofautiana.

Mbunge huyo ambaye alilala polisi kwa siku mbili, Jumatatu iliyopita alipandishwa kizimmbani na kusomewa mashtaka ya jaribio la kuua kwa kukusudia.

Pia Soma

Advertisement
Hata hivyo, mbunge huyo alikana mashtaka hayo na kurudishwa rumande kabla ya kuwasilisha ombi lake la kutaka Mahakama hiyo impatie dhamana.

Inaelezwa kuwa DJ huyu kwa sasa anaendelea kupata matibabu katika hospitali moja mjini Nairobi baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuondolea risasi iliyompata shingoni.

Kesi hiyo imekuwa ikifuatiliwa na wengi katika mitandao ya kijamii nchini Kenya ambako wengi walionyesha kiu ya kujua hatma ya mbunge huyo.

Kesi ya Babu owino inawadia wakati ambao polisi imetangaza kutotoa tena ulinzi kwa viongozi wa Serikali ambao wanakabiliwa na kesi za uhalifu.

Chanzo: mwananchi.co.tz